Articles by "M"
Showing posts with label M. Show all posts

 


📌 Anadi soko la mazao jamii ya mikunde India

📌 Mnada mazao ya kunde mtandaoni waboresha biashara ya kimataifa

📌 Biashara kati ya Tanzania na India kufikia dola bilioni 7.9

*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Serikali ya Tanzania imejidhatiti kuboresha na kuimarisha sekta ya kilimo kwa kuja na mipango kadhaa yenye lengo la kuongeza fursa kwa wakulima nchini.

Dkt. Biteko amesema hayo jijini New Delhi, India wakati akishiriki mkutano kuhusu masuala ya mazao jamii ya mikunde.

“Tunaongeza uwekezaji katika utafiti na kuboresha upatikanaji wa teknolojia za kisasa za kilimo ambapo kila afisa wa ugani nchini amepewa vifaa vyote muhimu ikiwemo pikipiki na kompyuta ili kutoa huduma nzuri na kwa wakati kwa wakulima wetu.” Amesema Dkt. Biteko

Amesema Serikali pia imeboresha shughuli za usafirishaji wa bidhaa ikiwa ni pamoja na kurahisisha michakato ya uuzaji mazao "Tanzania inaendeleza ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) ambayo itaimarisha usafirishaji wa bidhaa yenye urefu wa takribani kilomita 500 kutoka Bandari ya Dar es Salaam hadi Dodoma ambayo imekamilika na na inatumika.

Vilevile, amesema kupitia mradi wa BBT (Building a Better Tomorrow) Serikali imewezesha vijana kwa kuwapa ardhi, fedha na upatikanaji wa masoko sambamba na kuongeza huduma za kifedha za kidijitali.

Aidha, Dkt. Biteko amesema “India ni soko muhimu kwa mazao jamii ya kunde kutoka Tanzania na tunaweza kupata mafanikio makubwa zaidi. Leo nawaalika wawekezaji kutoka India na nchi nyingine duniani kuja kuwekeza katika sekta ya kilimo ya Tanzania kuanzia uzalishaji wa kisasa wa soya hadi uwekezaji katika mifumo ya usimamizi wa mavuno,”

Akizungumzia maendeleo ya sekta mazao jamii ya mikunde, amesema kuwa mwaka 2023, Tanzania ilizalisha takriban tani 250,000 za mbaazi, ikiwa ni ongezeko la asilimia 56 ikilinganishwa na mwaka 2018.

Inakadiriwa ifikapo mwaka 2030 Tanzania itakuwa na ukuaji mkubwa katika Pato la Taifa kupitia Kilimo, ambapo mauzo ya maharage mekundu, mbaazi na choroko yanatarajiwa kufikia dola bilioni 1.47, dola milioni 84 na dola milioni 115. Aidha, ili kufikia uwezo huo, Tanzania imeweka mikakati ya kukuza sekta ya mazao jamii ya kunde kupitia Mfumo wa Stakabadhi Ghalani kwa wakulima kusajiliwa, kuboresha mbinu za kilimo na teknolojia, kuhakikisha ubora na viwango vya mazao kulingana na mahitaji ya soko.

Pamoja na hayo Dkt. Biteko amesema “Mazao jamii ya kunde nchini Tanzania yanauzwa kupitia mnada wa mtandaoni ambao unatoa fursa kwa wafanyabiashara kupata taarifa kuhusu mizigo iliyohifadhiwa katika ghala lililosajiliwa,”

Amesisitiza “Mfumo huu unahakikisha uwazi, ufuatiliaji na ufanisi katika biashara ya kimataifa. Mwaka 2024 pekee kupitia mfumo huu, wakulima wa Tanzania walipata zaidi ya dola milioni 91.31 kutoka katika biashara ya mbaazi, dengu na maharagwe ya soya, ubunifu huu si tu unaimarisha ushindani wetu bali pia unafungua fursa mpya za ushirikiano,”

Kufuatia hali hiyo,kiwango cha biashara kati ya nchi hizo mbili kimeongezeka na kufikia dola bilioni 7.9 kwa mwaka wa fedha 2023/2024. Pia, mwaka 2023 mauzo ya mbaazi kutoka Tanzania kwenda India yalifikia tani 186,447 yenye thamani ya dola milioni 139.1

Daraja la Jordani lililopo Kata ya lemara Mtaa wa levolosi lakamilika kwa Asilimia 70 huku mkandarasi akisema ndani ya wiki mbili zijazo litakuwa tayari kwa matumizi 

Akizungumza wakati wa Ukaguzi wa Ujenzi wa kivuko hicho Diwani wa Kata ya lemara Naboth Silasie amesema ni faraja kwao kupatikana kwa kivuko cha jordani kwani  kinaunganisha mitaa miwili ambapo ni Elikirowa na Mtaa wa olepolosi

Amesema kuwa upatikanaji wa kivuko hicho ni Kutokana na jitihada za kujenga hoja kwenye ngazi ya Mtaa na Jimbo ambapo mahitaji yalikuwa ni kujengwa kwa madaraja matatu ambapo ni Daraja la Mungu, Daraja la Jordani na Daraja la Elikirowa

Amesema kuwa kivuko cha Daraja la Mungu tayari kimekamilika ambapo Shilingi Milioni sabini na tano  kutoka TASAF zilitumika kwenye Ujenzi huo

Sambamba na hilo Naboth amesema Kwa upande wa kivuko cha Jordani fedha zilizotolewa kutoka katika mfuko wa Jimbo ni Shilingi Milioni kumi ambapo zinatumika kukamilisha Ujenzi huo

Amesema hapo awali wakazi wa maeneo hayo walikuwa wanashindwa kuvuka hasa watoto na waendesha pikipiki ambao iliwalazimu kuzunguka upande wa pili kwani ukifika wakati wa Mvua eneo hilo huwa halipitiki

Pia amewaomba wananchi wa Mtaa wa levolosi kukipokea kivuko hicho huku akitoa rai kwa wakazi wa maeneo hayo kuonyesha ushirikiano katika kutunza kivuko hicho kwani Serikali haiwezi kufanya Kila kitu bila ya ushirikiano na wananchi

Nae Mwenyekiti wa Mtaa wa levolosi Rashida Shabani amesema kivuko kilichokuwepo hapo awali kilikuwa ni mbao ambapo wananchi na watoto walikuwa wanaanguka wakati wakipita katika Daraja hilo

Amesema juhudi za Diwani wa Kata hiyo Naboth Silasie zimezaa matunda kwani Daraja hilo mpaka Sasa limefiki asilimia 70 ingawa changamoto iliyopo  eneo hilo ni tindiga hivyo kadri wanavyozidi kuchimba udongo unaanguka naMaji yanatoka mengi huku akitoa rai kwa mkandarasi kuongeza kazi kukamilisha kivuko hicho kwani tunaelekea msimu wa mvua nyingi

Nae Mkandarasi anaejenga Daraja hilo la Jordani amesema KAZI imefikia asilimia 70 na asilimia 30 imebakia kufunika juu Ili watu waanza kupita

Amesema kwa asilimia zilizobaki atatumia wiki mbili kukamilisha kazi yote kwani vifaa vyote vipo huku akiomba kuletewa mapema vifaa vilivyobaki kwa wakati.