
Na Mwandishi wa OTR
Pwani. Serikali imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi kwa kutengeneza mazingira rafiki ya biashara na uwekezaji kupitia mifumo yenye ufanisi, kupunguza urasimu usio wa lazima, kuboresha utoaji wa huduma na kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi katika kuunga mkono utekelezaji wa Dira 2050.
Wito huo ulitolewa Ijumaa jioni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, wakati akifunga awamu ya tatu ya Programu ya Mafunzo Elekezi ya siku nne kwa Watendaji Wakuu wa Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha mkoani Pwani.
Akizungumza na viongozi hao, Mhe. Kikwete alisema mafanikio ya Dira 2050 hayatategemea ubora wa sera na mipango pekee, bali namna taasisi za umma zitakavyotekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuzalisha matokeo yanayoonekana kwa wananchi na kwa uchumi wa Taifa.
Amewataka Wakuu wa Taasisi za Umma kuhakikisha taasisi wanazoziongoza zinachangia kutengeneza mazingira rafiki ya biashara na uwekezaji kupitia utoaji wa huduma wenye ufanisi, ubunifu na ushirikiano mkubwa na sekta binafsi.
Alisema taasisi za umma zinapaswa kuwa wawezeshaji wa maendeleo badala ya kuwa vikwazo kwa wawekezaji, kwa kuwa ubora wa huduma zinazotolewa una mchango mkubwa katika kuvutia uwekezaji, kuongeza ushindani wa uchumi na kufungua fursa mpya za maendeleo.
Alisisitiza kuwa uongozi wa Watendaji Wakuu utapimwa kwa uwezo wao wa kuondoa vikwazo vinavyokwamisha biashara na uwekezaji, kuboresha utoaji wa huduma, kuongeza tija na kujenga taasisi zinazowajibika kwa wananchi.
"Uongozi wenu utapimwa si kwa mipango mizuri pekee, bali kwa uwezo wa kuitekeleza, kuondoa urasimu usio wa lazima, kuboresha utoaji wa huduma, kuongeza tija na kujenga taasisi zinazowajibika kwa wananchi," alisema.
Aliongeza kuwa kila taasisi ya umma inapaswa kutambua kuwa maamuzi yake yana athari ya moja kwa moja katika mazingira ya biashara na uwekezaji, hivyo kila mchakato wa utoaji huduma unapaswa kujenga imani kwa wawekezaji na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa.
"Wajibu wenu wa msingi ni kuhakikisha Dira 2050, iliyoanza kutekelezwa rasmi Julai Mosi mwaka huu, inageuzwa kuwa matokeo yanayoonekana kupitia taasisi mnazoziongoza,” alisema.
“Nina matarajio kuwa utekelezaji wa Dira 2050 utakuwa sehemu ya ajenda ya kudumu katika maamuzi na majukumu yenu ya kila siku.”
Alisema mipango, mikakati na utekelezaji wa taasisi za umma lazima viendane na malengo ya Dira 2050 ili kuchochea maendeleo ya Taifa.
"Mtakapotekeleza majukumu yenu kwa weledi, uwajibikaji na ufanisi, matokeo chanya yatapatikana na yatachangia kufanikisha maono ya Taifa," alisisitiza.
Aidha, aliwataka Watendaji Wakuu kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi, wadau wa maendeleo na wananchi ili kuongeza thamani ya huduma zinazotolewa na taasisi zao.
Alisema ushirikiano huo utasaidia kujenga mifumo inayowawezesha wafanyabiashara kufanya shughuli zao kwa ufanisi zaidi, wawekezaji kupata huduma kwa wakati na taasisi za umma kuchangia kikamilifu katika kukuza uchumi.
Mhe. Kikwete pia alizitaka taasisi za umma kutumia mifumo ya kidijitali, kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani, kuboresha utawala bora na kuhakikisha viashiria vya utendaji vinaakisi malengo ya Dira 2050.
Alieleza kuwa mafanikio ya mafunzo hayo hayatapimwa kwa idadi ya vyeti vilivyotolewa, bali kwa mabadiliko yatakayoonekana katika taasisi wanazoziongoza washiriki, ikiwemo utoaji bora wa huduma, matumizi yenye tija ya rasilimali za umma, ongezeko la mapato na uwajibikaji mkubwa.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Wizara ya Mipango na Uwekezaji anayeshughulikia Uwekezaji, Dkt. Fred Msemwa, alisema mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka ambapo Tanzania imeingia katika kipindi muhimu cha mageuzi ya kiuchumi yanayolenga kukuza uchumi wa Taifa hadi kufikia takribani mara kumi ya ukubwa wake wa sasa kupitia utekelezaji wa Dira 2050.
Alisema mazingira hayo yanahitaji viongozi wenye maono, ubunifu na uwajibikaji watakaoweza kutafsiri malengo ya kitaifa kuwa matokeo ya kiuchumi na kijamii yanayopimika.
"Nina imani kuwa maarifa mliyoyapata kupitia mafunzo haya pamoja na uzoefu mliobadilishana yatawaongezea uwezo na utayari wa kutekeleza majukumu yenu kwa ufanisi zaidi," alisema.
Aliongeza kuwa katika kipindi hiki cha mageuzi makubwa ya uchumi, uongozi wenye maono, ubunifu na uwajibikaji utakuwa nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya Dira 2050, akieleza kuwa taasisi za umma zina nafasi ya kipekee katika kuweka mazingira yatakayochochea uwekezaji, uzalishaji na ushindani wa uchumi wa Tanzania.
Kwa upande wake, Bw. Ibrahim Mahumi, aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, alisema kuimarisha uwezo wa uongozi wa Watendaji Wakuu ni msingi muhimu wa kuboresha ubora wa huduma za umma na kuhakikisha taasisi hizo zina uwezo wa kutekeleza kwa ufanisi vipaumbele vya maendeleo ya Taifa.
Bw. Mahumi alisema viongozi hao wana wajibu wa kujenga utamaduni wa weledi, uwajibikaji na utendaji unaozingatia matokeo katika taasisi wanazoziongoza, akisisitiza kuwa uongozi madhubuti ni msingi wa kujenga taasisi zinazotoa huduma bora kwa wananchi.
Aliongeza kuwa maarifa na uzoefu walioupata washiriki kupitia mafunzo hayo yanapaswa kutafsiriwa kuwa hatua za vitendo kupitia kuboresha maamuzi ya kiutendaji, kuimarisha mifumo ya uongozi na kuongeza ufanisi katika usimamizi wa rasilimali za umma.
Akitoa mtazamo wa taasisi zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina, Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, alisema mageuzi yanayoendelea katika taasisi za umma tayari yameanza kuzaa matunda kupitia kuboreshwa kwa utoaji wa huduma, kuongezeka kwa ufanisi wa kiuchumi na kuimarika kwa utendaji wa taasisi nyingi za umma.
Kwa sasa, Serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina inasimamia taasisi za umma na kampuni ambazo ina umiliki wa hisa chache 308 zenye thamani ya uwekezaji wa Sh92.3 trilioni, hali inayozifanya kuwa mhimili muhimu katika utekelezaji wa Dira 2050 na ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Kutokana na nafasi hiyo, Bw. Mchechu alisema mageuzi yanayoendelea yanaonesha kuwa taasisi hizo zina uwezo wa kuwa injini muhimu ya ukuaji wa uchumi endapo zitaendelea kuongozwa kwa misingi ya uwajibikaji, ubunifu na usimamizi bora wa rasilimali.
“Katika miaka ya hivi karibuni, taasisi za umma zimepiga hatua kubwa katika kuboresha utoaji wa huduma, kuongeza ufanisi wa kiuchumi na kuimarisha utendaji wake kwa ujumla,” alisema.
Alieleza kuwa mafanikio hayo yamewezesha baadhi ya taasisi kupunguza utegemezi wake kwa Mfuko Mkuu wa Serikali, hatua inayodhihirisha kuongezeka kwa uwezo wa kujitegemea kifedha na kuchangia zaidi katika maendeleo ya Taifa.
"Tunaendelea kusukuma ajenda maalumu ya mageuzi ili, baada ya muda, taasisi nyingi zaidi ziweze kujiendesha kwa mapato yao wenyewe, isipokuwa zile ambazo kwa asili ya majukumu yake zinapaswa kuendelea kupata ruzuku ya Serikali," alisema.
Bw. Mchechu alisema mafanikio ya mageuzi hayo hayapaswi kupimwa kwa takwimu za kifedha pekee, bali pia kwa mabadiliko ya fikra, utamaduni wa utendaji na uwezo wa viongozi wa taasisi hizo kusimamia mabadiliko.
"Kwangu mimi mafanikio haya siyo suala la namba pekee; ni suala la mtazamo, fikra na utamaduni mpya tunaouona ndani ya Bodi zetu na kwa Watendaji Wakuu. Uwezo tunaouona ni mkubwa, kujitoa kwao ni kwa kiwango kingine, na kila mmoja anaonesha kiu ya mabadiliko na mafanikio," alisema.
Alisema dhamira hiyo imeongeza umiliki wa mageuzi miongoni mwa viongozi wa taasisi za umma na kuweka msingi imara wa kufanikisha Dira 2050 kupitia taasisi zenye ufanisi, zinazojitegemea zaidi kifedha na zinazotoa mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2024, Programu ya Mafunzo Elekezi kwa Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma imewanufaisha takribani Watendaji Wakuu 244, ambapo viongozi 57 walishiriki katika awamu ya mwaka huu.
Programu hiyo huandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa kushirikiana na Taasisi ya UONGOZI ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kujenga viongozi wenye uwezo wa kuongoza taasisi za umma kwa ufanisi, kuimarisha utawala bora, kuboresha huduma kwa wananchi na kuhakikisha Dira 2050 inatafsiriwa kuwa matokeo halisi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.







Siku moja, marafiki zangu wawili wa karibu niliowaamini sana walikuja kunipiga mzinga wa kuazima gari hilo kwa masaa machache tu, wakidai wana dharura kubwa ya kifamilia mji wa jirani.
Kwa roho safi na urafiki wetu wa miaka mingi, niliwakabidhi funguo bila wasiwasi wowote. Hata hivyo, masaa machache yaligeuka kuwa siku. Walipokosa kurudi jioni ile, nilianza kuwapigia simu lakini zote zilikuwa zimezimwa.
Siku ya pili na ya tatu zilipopita bila kuona gari wala kupata habari zao, ndipo mshtuko na ukweli mchungu uliponipiga marafiki zangu walikuwa wamenigeuka na kutoweka na gari langu!
Nilienda kutoa taarifa kituo cha polisi, lakini siku zilivyozidi kusonga, ufuatiliaji wao haukuzaa matunda yoyote na matumaini yangu ya kumpata chombo changu yalianza kuyeyuka. SOMA ZAIDI.
Kati ya vitu vyote, jicho langu lilivutiwa na pete moja ya chuma cha ajabu iliyokuwa na mchoro wa kipekee. Mzee yule alinitazama kwa tabasamu fumbo kisha akasema, “Chukua hii kijana, itakusaidia.” Niliinunua kwa fedha kidogo sana nikiamini ni urembo wa vidole tu.
Nilipoivaa tu mkononi, sikuichukulia maanani. Lakini haikupita hata siku mbili, mambo ya ajabu yalianza kutokea katika maisha yangu ya kila siku mambo ambayo sikuwahi kuyatarajia kabisa. SOMA ZAIDI.
Kila nilipoona marafiki na vijana wenzangu wakipata fursa za kusafiri na kuendelea kimaisha, nilijihisi aliyetupwa na aliyekataliwa. Wasiwasi na msongo wa mawazo vilianza kuitawala nafsi yangu, na nilianza kuamini kuwa labda nyota yangu ya mafanikio ilikuwa imefungwa kabisa. SOMA ZAIDI.
Ndoa yetu ilianza kwa amani na matumaini makubwa ya kujenga familia yenye furaha. Hata hivyo, miaka ilipozidi kusonga bila kupata mtoto, furaha hiyo ilianza kutoweka taratibu.
Baada ya miaka minane ya ndoa, tulikuwa tumetembelea hospitali na zahanati mbalimbali, tukafanya vipimo vyote vilivyowezekana, lakini madaktari walizidi kutuambia hakuna tatizo la kibiolojia linaloonekana.
Aibu na maneno ya kejeli kutoka kwa baadhi ya ndugu na majirani yalianza kutuandama. Wengi walimnyooshea mke wangu kidole, na hata wengine walinishauri nimfukuze na kuoa mwanamke mwingine.
Mke wangu alilia kila usiku, na mimi nilijikuta nikiwa sina la kufanya huku nikishuhudia amani na matumaini ya familia yetu yakiporomoka. SOMA ZAIDI.
Baba yangu mzazi kabla ya kufariki dunia, aliniachia eneo kubwa la shamba la urithi kama mtoto wake wa pekee wa kiume ili liwe msingi wa maisha yangu na familia yangu.
Hata hivyo, baada tu ya mazishi yake kuisha, wajomba na ndugu wa karibu walianza kuweka mpango wa kuninyang’anya haki hiyo.
Walitengeneza nyaraka za uongo, wakadai kuwa baba hakuwahi kumiliki eneo hilo peke yake, na kunifungulia kesi iliyodumu mahakamani kwa miaka kumi mtawalia.
Kwa miaka hiyo yote kumi, nilitumia akiba yangu yote kulipa mawakili na gharama za kesi. Kila mara tulipokaribia kufanya maamuzi, kesi iliahirishwa au nyaraka muhimu zilipotea kimiujiza.
Ndugu hao walitumia fedha na ushawishi wao kuninyanyasa, huku mimi nikibaki maskini wa kutupwa na mwenye msongo mkubwa wa mawazo. Nilihisi kutengwa na kudhulumiwa jasho la marehemu baba yangu.SOMA ZAIDI.
Tafadhali Zingatia: Ikiwa unasoma kwenye PHOENIX, tafadhali bofya kitufe cha “Soma Makala Asili” kilicho upande wa juu kulia ili kusoma makala kamili.
Binti yangu alikuwa mtoto mwenye bidii na mwenye kuonyesha uwezo mkubwa wa akili darasani wakati wa vipindi vya kawaida. Walimu walimsifu kwa ustahimilivu na uwezo wake wa kuelewa masomo kwa haraka.
Hata hivyo, kuanzia alipoingia darasa la sita, kulizuka mtihani mzito uliotatiza maisha ya familia yetu. Kila siku ya mtihani ilipofika, binti yangu alipata homa kali ya ghafla, maumivu makali ya tumbo, na kupoteza kuona vizuri kiasi cha kushindwa hata kushika kalamu.
Tulitembelea hospitali mbalimbali na kufanya vipimo vya kila aina, lakini madaktari walithibitisha kuwa mwili wake haukuwa na ugonjwa wowote wa kimatibabu.
Hali hii ilipojirudia kwa miaka miwili mtawalia, matokeo yake ya shule yaliporomoka vibaya mno, na alianza kuogopa hata kwenda shule. SOMA ZAIDI.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus C. Sangu, akizungumza na waandishi wa habari mjini Sumbawanga, Mkoa wa Rukwa, leo Julai 23, 2026,kuhusu Tanzania kushiriki katika maonesho ya Wajasiliamali Wadogo (Juakali) ya Afrika Mashariki yatakayofanyika Kigali Rwanda mwezi Oktoba mwaka huu.
Na: Mwandishi Wetu, SUMBAWANGA
Serikali imetangaza kuwa Tanzania itashiriki Maonesho ya 26 ya Wajasiriamali Wadogowadogo, Wadogo na wa Kati (MSMEs) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, maarufu kama Nguvu Kazi/Jua Kali, yatakayofanyika jijini Kigali, Rwanda kuanzia Oktoba 30 hadi Novemba 8, 2026.
Akitoa taarifa kwa umma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, amesema Tanzania itawakilishwa na wajasiriamali 250 kati ya washiriki wapatao 1,000 wanaotarajiwa kutoka nchi nane wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Amesema kaulimbiu ya maonesho ya mwaka huu ni "Kuendeleza Mnyororo wa Thamani kwenye Sekta ya Ngozi na Kilimo cha Bustani (Matunda na Mbogamboga) katika Ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki."
"Maonesho hayo yanalenga kuwawezesha wajasiriamali kurasimisha shughuli zao za biashara, kutangaza bidhaa na huduma, kubadilishana uzoefu, kuongeza ujuzi wa uzalishaji pamoja na kupanua masoko ya bidhaa na teknolojia za uzalishaji."amesema Waziri Sangu
Ameongeza kuwa ushiriki wa Tanzania katika maonesho hayo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha sekta ya ujasiriamali, kukuza biashara za ndani na nje ya nchi, pamoja na kuongeza fursa za ajira zenye staha kwa Watanzania.
Aidha, Waziri Sangu amewataka wajasiriamali wenye sifa kutumia fursa hiyo kwa kujisajili kushiriki maonesho hayo kuanzia sasa hadi Septemba 30, 2026 kupitia mfumo rasmi wa usajili uliotengwa kwa ajili ya washiriki.
Maonesho ya Nguvu Kazi/Jua Kali ni miongoni mwa majukwaa makubwa ya biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki yanayowakutanisha wajasiriamali, wawekezaji na wadau wa maendeleo kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kuongeza ushindani wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya ukanda huo.
Ripoti zake za shule zilianza kuonyesha maksi za chini sana, alipoteza hamu ya kusoma, na walimu wake walianza kulalamika kuwa anakaa darasani akiwa amezubaa na kukosa ushirikiano.
Nilitumia fedha nyingi kumlipia walimu wa ziada (tuition) na kununua vitabu vya kila aina, lakini hakuna kilichobadilika. Kila mtihani uliporudi, matokeo yalikuwa mabaya zaidi kuliko ya nyuma.
Nilianza kuchanganyikiwa na kuhisi kuwa siku za usoni za mwanangu zinasambaratika mbele ya macho yangu. SOMA ZAIDI.
Urafiki wa miaka mingi unaweza kukudanganya ukadhani unamjua mtu kwa undani. Rafiki yangu wa karibu, niliyemwamini na kushirikiana naye kwa kila jambo, alinigeuka kwa namna mbaya zaidi.
Siku moja nilipokea simu kutoka kwa taasisi ya mikopo wakinidai fedha nyingi ambazo sikuwahi kuzikopa. Baada ya kufuatilia, nilipata mshtuko mkubwa.
Baada ya kugundua kuwa rafiki yangu alitengeneza nyaraka za uongo na kutumia kitambulisho changu kukopa mamilioni ya fedha, kisha akatoweka na kukata mawasiliano.
Riba zilianza kuongezeka, na watoa mikopo walianza kunitishia kunipiga mnada na kunichukulia hatua za kisheria. Nilipoteza amani ya moyo, sikuweza kulala usiku, na jina langu lilikuwa hatarini kuchafuka kabisa kwa kosa ambalo sikufanya. SOMA ZAIDI.
Kwa miaka saba mtawalia, nilikuwa mfanyakazi wa mfano kwenye kampuni yetu. Nilijitolea kwa moyo wote, nikifanya kazi hadi usiku wa manane na kuacha familia yangu nyuma ili kuhakikisha kampuni inapata faida.
Hata hivyo, uaminifu wangu haukuthaminiwa. Siku moja niliitwa ofisini kwa Mkurugenzi na kupewa barua ya kufukuzwa kazi mara moja, kisa ikiwa ni fitina zilizotengenezwa na bosi mpya aliyekuwa ananionea wivu.
Nilipoteza kila kitu kwa sekunde moja. Bado nilikuwa na madeni ya benki, kodi ya nyumba ilikuwa inakaribia kuisha, na watoto wangu walihitaji ada za shule. Kwa miezi miwili ya mwanzo, maisha yaligeuka kuwa usiku mnene.
Nilihisi kuchezewa akili, kupotezewa muda wangu, na kukatishwa tamaa na mfumo mzima wa maisha.SOMA ZAIDI.
Badala ya kukata tamaa na kuitumia kwa chakula cha siku mbili, niliamua kuchukua hatua ya kipekee nilinunua bidhaa ndogo za viungo na kuanza kuzitembeza mtaani nyumba kwa nyumba.
Maisha ya biashara ya mtaji mdogo hayakuwa mepesi. Nilitembea umbali mrefu chini ya jua kali, nilipatwa na dharau na kukatishwa tamaa na watu wengi.
Kwa miezi kadhaa, biashara ilikuwa ikienda kwa kusua sua mno; faida niliyopata ilikuwa ndogo sana kiasi cha kushindwa hata kukuza mtaji wangu. Nilijihisi kama ninazunguka kwenye duara lile lile bila kupiga hatua.









