Mawaziri wa Mawasiliano kutoka Tanzania na Kenya wamezindua rasmi maunganisho ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) wa Tanzania unaosimamiwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), na mikongo ya baharini ya Mombasa kupitia Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (ICTA).

Uzinduzi huo umefanywa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Uchumi wa Kidigitali wa Kenya, Injinia William Kabogo Gitau, pamoja na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania, Mhe. Jerry Silaa.

Mawaziri hao wamesisitiza kuwa hatua hiyo ni ya kihistoria, ikilenga kuimarisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano ya uhakika, pamoja na kupunguza changamoto za kukatika kwa mtandao.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Gitau amesema: “Jambo la msingi ni ushirikiano wa dhati kati ya nchi zetu mbili. Ni muhimu kuhakikisha tunatunza miundombinu hii ya kimkakati ili kuepuka uharibifu unaoweza kusababisha kukatika kwa umeme na mtandao. Pia tuendelee kuimarisha mahusiano yetu kwa manufaa ya pande zote.”

Kwa upande wake, Mhe. Jerry Silaa alisema kuwa ujenzi wa miundombinu ya pamoja ya mawasiliano kati ya nchi washirika ni wajibu wa pamoja kwa ajili ya maendeleo ya kikanda.

“Kuna faida kubwa ya kuwa na maunganisho mengi ya mikongo ya mawasiliano. Hii husaidia kuwepo kwa mtandao wa uhakika, unaotegemewa hata wakati wa changamoto za kiufundi katika njia moja ya mawasiliano,” alisema Silaa.

Mkongo huo tayari umeanza kufanya kazi nchini Kenya, hatua inayowezesha huduma za intaneti na mawasiliano kusambaa kwa kasi zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Uzinduzi huu unaashiria mafanikio makubwa katika juhudi za kuunganisha ukanda huu kidigitali na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.










  


Jina langu ni Simon kutoka kaunti ya Vihiga, nilikuwa mfanyibishara haswa wa kilimo, nilikuwa na ng’ombe wawili wa maziwa ambao walikuwa wananipa faida kubwa sana kutokana na uuzaji wa maziwa.

ilifanya pia ukulima wa nyanya lakini uuzaji maziwa ulikuwa na faida sana kulinganisha na kilimo cha nyanya, kazi hii iliniwezesha kulipia wanangu karo ya shuleni, kuwezesha wanangu kupata lishe bora na hata kufanya maendelea mengi pale nyumbani.


Ng’ombe wangu walikuwa wenye afya kutokana na mimi kujua ni kipi haswa walihitaji ili kuleta faida, ila siku moja niliamka na kukuta zizi la ng’ombe langu lilikuwa wazi.

Kufumba na kufungua macho hapakuwa na mifugo wangu niliowategemea, nilikumbwa na mshutuko wa moyo na hata nilidhani kwamba walikuwa tu karibu, kumbe walikuwa tayari wameshaibiwa. Soma zaidi hapa. 

Jumla ya Washiriki 700 kutoka taasisi mbalimbali za Tanzania bara na Visiwani,wanatarajiwa kuhudhuria mkutano mkuu wa kwanza wa mwaka wa Jumuiya ya Wataalamu wa Usimamizi wa Rasilimali watu na utawala katika utumishi wa umma (TAPA-HR ),Unaotarajia kufanyika katika Ukumbi wa kimataifa wa Aicc MkoaninArusha.

Mkutano huo utaanza rasmi Julai  22-25,2025 na kufunguliwa na Waziri wa nchi  Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala bora Mh George Simbachawene .

Akizungumza na vyombo vya habari mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya mkutano huo bi.Grace Meshy amesema mkutano huo una lengo la kubadilishana uzoefu katika maswala mbalimbali katika utawala pamoja na kukuza ujuzi na  uweledi na maadili  katika maswala ya rasilimali watu pamoja na utawala.

"Tunafahamu kuwa kada yetu ni kioo cha jamii hivyo tunatarajia kuwa tutaendelea kukumbushana  maadili na kubadilisha uzoefu kwa kuwa jukwaa hili ni la kwanza kufanyika hivyo mambo mazuri yanakuja kwa kuwa sisi ni vioo  katika taasisi zetu"Alisema bi.Meshy

Kauli mbili ya mkutano huo ni mwelekeo mpya wa nafasi ya wataalamu wa usimamizi wa rasilimali watu na utawala kusukuma mabadiliko kuendana na mageuzi ya teknolojia kwaajili ya kuboresha huduma katika utumishi wa umma

Pia  mkutano huo  unalenga kuwakutanisha wataalamu wa kada ya usimamizi wa rasilimali watu na utawala katika utumishi wa umma Kutoka Tanzania bara na visiwani ili  kuwajengea uwezo na  kuleta tija katika kufikisha  malengo makuu ya taasisi zao na ustawi wa wananchi kwa ujumla.

Amewataka  waajiri wote ambao wapo katika wizara mbalimbali Mamlaka za serikali za mtaa, wakala wa serikali pamoja na idara zinazojitegemea kuendelea kuwawezesha wataalamu kuweza kushiriki mkutano huo muhimu .











 


Na Mwandishi wetu- Dodoma


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amewapongeza watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku kwa maendeleo ya Taifa.


Dkt. Yonazi ameyasema hayo leo tarehe 18 Julai, 2025 Ofisini kwake jijini Dodoma akikabidhiwa tuzo na  Mkurugenzi wa Idara ya Uwezeshaji Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi Bw. Conrad Milinga iliyotolewa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati akifungua Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Sabasaba 2025.



Alisema Ofisi ya Waziri Mkuu kupokea tuzo kumeongeza motisha katika ushiriki wa maonesho yajayo makubwa ya Kimataifa ya Sabasaba  na kutambua mchango wa Ofisi hiyo iliyoutoa kwa wananchi katika kipindi chote cha maonesho hayo na kutambua huduma ianayotolewa kwa wananchi.

“Ofisi ya Waziri Mkuu imefurahi sana kupokea tuzo hii kama ishara ya kutambua ushiriki wetu na mchango ambao Ofisi yetu inatoa kwa wananchi hivyo tunaamini ushiriki wetu unaofuata utakuwa wa viwango vya juu sana,” Alisema Dkt. Yonazi.



Pia  aliishukuru Serikali kwa juhudi kubwa inazofanya chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) ambayo ndio mratibu wa Maonesho kwa  kuhakikisha maonesho hayo yanaleta tija na mageuzi makubwa katika sekta ya kiuchumi kwa wananchi na Kimataifa.


“Tunazishukuru sana Taasisi mbalimbali ambazo tumeshirikiana nazo na viongozi ambao wameendelea kutupa maelekezo yaliyowezesha kufanya vizuri katika maonesho hayo na tunaamini kwamba tutaendelea kuwa washindi au hata washindi wa jumla,”Alishukuru.

Ikumbukwe Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Sabasaba 2025 yalifunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi tarehe 07 Julai, 2025 na kufungwa na Waziri Mkuu Mhe.  Kassim Majaliwa  katika viwanja vya maonesho Sabasaba jijini Dar es Salaam Julai 13, 2025.

 

Niliwahi kujaribu kila aina ya biashara kuuza miwa, kuuza viatu, hata kufungua duka la juisi lakini zote zilidumu kama ndoto ya usiku. Mwezi mmoja, miwili, tayari biashara imeshakufa.

Wateja walikuwa wachache, faida haikupatikana, na kila mara nilijikuta nikipoteza mtaji na kuanza upya. Ilifika hatua nikaamini kuwa bahati haikuwa upande wangu kabisa.

Watu walinicheka, wengine walinionea huruma, na familia ilianza kunisihi nitafute ajira badala ya kupoteza pesa kwenye biashara zisizo na tija. Lakini moyoni nilijua kuna kitu kilikuwa kinakwamisha mafanikio yangu.


Niliona watu wengine wanaanzisha biashara ndogo ndogo na ndani ya miezi sita wanapanuka lakini mimi kila jambo lilikuwa kama limefungwa kwa kamba isiyokatika. Nilianza kufanya utafiti kuhusu hali yangu, nikasoma kuhusu nyota, nguvu za bahati, na njia za kufungua milango ya mafanikio.

Siku moja, nikiwa kwenye mitandao ya kijamii, nilikutana na ushuhuda wa kijana mmoja aliyekuwa na hali kama yangu. Alieleza jinsi alivyosaidiwa kufungua nyota yake ya biashara kupitia msaada wa kitaalamu wa kiroho. Soma zaidi hapa. 


 


Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa shilingi Bilioni 19.6 kwa ajili ya Mradi wa Kuboresha Ubora wa Elimu ya Sekondari SEQUIP mkoani Njombe.

Kati ya fedha hizo jumla ya Shilingi Bilioni 4.360 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo majengo ya madarasa, maabara, mabweni, Bwalo la chakula Jengo la Utawala na nyumba za walimu katika shule ya Sekondari ya wasichana ya mkoa wa Njombe ambayo imekamilika.

Hayo yamebainishwa tarehe 17 Julai 2025 na Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Njombe Mwl Nelasi Mulungu ambapo amesema pia Bilioni 1.6 imetolewa kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya Mkoa ya Amali ambayo inaendelea na ujenzi katika Wilaya ya Ludewa.

Mwl Mulungu amesema kuwa serikali imetoa zaidi ya Bilioni 12.638 kwa ajili ya ujenzi wa shule 20 za kata katika mkoa huo wa Njombe.

Pia amesema kuwa serikali imetoa zaidi ya Shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mingine katika mkoa wa Njombe ikiwemo ujenzi wa Mabweni, Nyumba za walimu, na Matundu ya vyoo






.

 


Nilikuwa nimekata tamaa. Wote tuliomaliza shule pamoja walikuwa wameshapata ajira nzuri au walikuwa wanaendelea na masomo ya juu. Mimi nilibaki kijijini, nikiuza duka dogo ambalo halikuwa linaingiza hata ya chakula ya siku. Sikuamini sana kwenye ndoto zangu tena, kwa sababu kila mlango niliogonga ulinifungiwa kwa jibu moja: “Huna qualifications.”

Nilijaribu kujiunga na mafunzo ya ufundi, lakini sikuweza kumaliza kwa sababu ya ada. Nilijitahidi kwa biashara, lakini kila mara nilipokuwa karibu kupata wateja, jambo la ajabu lilitokea: bidhaa zinaharibika, mtu anafungua duka lingine mbele yangu, au nalazimika kuuza bidhaa kwa hasara. Ilikuwa kama mikosi ilinifungia njia zote.


Ilifika hatua nilianza kuamini kwamba bahati yangu haipo. Siku moja nikiwa nimekaa kwa stoo yangu ndogo nikitafakari, niliona status ya jamaa mmoja Facebook ambaye tulikuwa naye shule. Alikuwa anasherehekea kufungua duka lake la tatu jijini, na aliandika maneno haya: “Sio kila kitu ni elimu, kuna wengine wanasaidiwa kwa ujuzi wa kipekee.” Soma zaidi hapa. 

 

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imekutana kujadili utekelezaji pamoja na kupitisha Mpango Kazi wa Awamu ya Pili ya Mradi Kabambe wa Kuboresha Takwimu nchini (Tanzania Statistical Master Plan-TSMPT II).

 

Kikao hicho cha kujadili mradi wa TSMPT II kimefanyika jijini Dodoma jana chini ya mwenyekiti wake ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt Natu El-maamry Mwamba. Mradi huo wa TSMPT II unatekelezwa katika kipindi cha mwaka 2022/23 hadi 2026/27.

 

Awamu ya kwanza ya utekelezaji Mradi Kabambe wa Kuboresha Takwimu nchini (TSMPT I) ulifanyika katika kipindi cha mwaka 2011/12 hadi 2017/18.

 

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) mbali na mambo mengine ina jukumu la kutoa takwimu rasmi zilizo bora na huduma zinazokidhi mahitaji ya wadau wa kitaifa na kimataifa kwa ajili ya kupanga mipango na kufanya maamuzi yenye uthibitisho.

  

Jina langu ni Jesca kutokea Tanga, ninakoishi na familia yangu, nimeolewa na mwanaume mzuri anayefanya kazi na chombo cha habari huko Dar es Salaam, wakati mimi nafanya kazi katika Hoteli moja jijini hapa.

Kufanya kazi katika hoteli sio rahisi kwani kila siku narudi nyumbani nikiwa nimechoka sana na siwezi kumtunza mume wangu vizuri ingawa hajawahi kulalamika kuhusu hilo.

Hata hivyo, mwaka jana lilitokea jambo baya nyumbani kwetu likihusisha dada wa kazi na mume wangu, msichana huyu alichukua nafasi yangu kama mke, kuna kipindi hufua nguo zake za ndani na kuzianika bafuni ambapo mume wangu huoga pia.

Wanaume wengi kwa bahati mbaya wana udhaifu mkubwa hasa pale wanaopoona nguo ya mwanamke, mume wangu alijikuta amezama katika penzi na dada wa kazi, wakawa wanafanya yao bila mimi kujua. Soma zaidi hapa

  


Siku zote nilijua ninataka kuwa mama. Nililelewa kwenye familia ya upendo, na ndoto yangu kubwa baada ya ndoa ilikuwa ni kulea mtoto wetu mwenyewe. Lakini mume wangu hakuwa na mtazamo huo.

Alinieleza mapema kabla ya ndoa kwamba kwa sasa hataki mtoto, na labda hata hana mpango wa kuwa mzazi kabisa. Nilidhani angetulia baada ya ndoa, lakini sikujua kwamba kauli hiyo ilikuwa ya kweli kabisa.

Tulipooana, mwaka wa kwanza ulipita na nilipojaribu kuleta mada ya mtoto, alikwepa. Mwaka wa pili, alikua mkali zaidi. Alisema wazi: “Mimi sitaki mtoto. Nisingependa kulea dunia hii ilivyo.” Maneno hayo yalinichoma.

Kila nikiona watoto wa rafiki zangu, kila ninapoona diaper kwenye duka, au baby shower kwenye Instagram, moyo wangu ulikua unazimia kwa ndani. Nilianza kuwa na huzuni isiyoisha.

Marafiki zangu walinijulisha kuwa huenda kuna jambo la ndani zaidi. Moja alinieleza: “Wanaume wengi wanaweza kubadilika, lakini kuna baadhi huwa wamefungwa kiroho wakiwa na sababu zisizoeleweka au mapingamizi ya maisha ya familia.” Akanishauri niwasiliane na watu walio na maarifa ya kusaidia kwenye masuala ya ndoa kiroho. Soma zaidi hapa.

 


Lengo ni Kuchochea Maendeleo, Usalama na Utunzaji wa Mazingira kwa Vizazi Vijavyo

Serikali kupitia Tume ya Madini imezindua mpango maalum wa “Uchimbaji Bora na Endelevu kwa Kizazi Kijacho”, unaolenga kuwawezesha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za uchimbaji madini nchini. Mpango huu unatoa fursa ya kuanzisha vikundi, kupata mikopo, pamoja na leseni za uchimbaji kwa lengo la kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Akizungumza katika mafunzo kwa wachimbaji wadogo yaliyofanyika katika vijiji vya Utaho A na Isalanda, Kata ya Kituntu na Puma mkoani Singida, Mjiolojia kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Geofrey Mutagwa, amebainisha kuwa mpango huo pia unalenga kuhakikisha kuwa shughuli za uchimbaji zinafanyika kwa usalama na kuzingatia utunzaji wa mazingira.

“Uchimbaji salama ni msingi wa maendeleo. Tunawafundisha wachimbaji si tu kuhusu mbinu bora za uchimbaji, bali pia umuhimu wa kulipa kodi ya serikali kama vile mrabaha wa asilimia 4 kwa madini ya ujenzi,” amesema Mutagwa.

Aidha, amewaonya wanaojihusisha na ununuzi wa madini bila kulipa kodi, akisisitiza kuwa mfumo wa malipo ya kodi unapatikana kupitia POS katika ofisi za madini. 

Amesisitiza kuwa kila mchimbaji ana wajibu wa kutoa taarifa za ukwepaji kodi kwa mujibu wa Kifungu cha 87 cha Sheria ya Madini, Sura ya 23, ili hatua za kisheria zichukuliwe.

Kwa upande wake, Mkaguzi wa Migodi na Baruti kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Eng. Lameck Maduhu, amesisitiza umuhimu wa usalama katika maeneo ya kazi.

“Fedha tunazopata zitakuwa hazina maana kama hatutajilinda. Ni lazima kuvaa vifaa kinga muda wote –  safety boots, kofia ngumu, suruali maalum na barakoa. Ndala hazihusiki kabisa kwenye machimbo,” ameeleza kwa msisitizo.

Ameongeza kuwa uchimbaji unaozingatia matumizi ya baruti unapaswa kufanywa kwa njia ya kitaalam na kwa uangalifu mkubwa ili kuzuia uharibifu wa mazingira, akihimiza wachimbaji kuacha tabia ya kukata na kuchoma miti kiholela.

Mchimbaji wa madini ya ujenzi kutoka Kijiji cha Utaho A, Jenifa Mtandu, ameishukuru Tume ya Madini kwa elimu waliyopewa, akisema imewapa maarifa ya kujilinda, umuhimu wa vikundi, na fursa za kupata mikopo kwa maendeleo ya shughuli zao.

“Mafunzo haya yametufungua macho. Tunajua sasa umuhimu wa leseni, kuwa na vikundi na mikopo. Tunaiona kesho yetu ikiwa salama zaidi,” amesema Mtandu kwa furaha.

Mpango huu umewezeshwa kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kwa lengo la kusaidia wachimbaji wadogo wa madini ya ujenzi hususan kokoto, ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya miundombinu, kuongeza kipato na kuchangia mapambano dhidi ya umasikini katika jamii.

Mpango huu unatarajiwa kuwa chachu ya mageuzi makubwa katika Sekta ya Madini nchini kwa kuhakikisha shughuli za uchimbaji zinafanyika kwa weledi, uadilifu, na kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.





Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira amewakumbusha watendaji wa Uchaguzi ngazi ya Mkoa na Jimbo kushirikiana na Wanahabari ili wananchi waweze kufahamu mambo mbalimbali yahusuyo Uchaguzi.

  


Naitwa David, tangu nilipoanza kufanya kazi katika shirika ambalo ninafanya kazi sasa, sikuwahi kupata nafasi ya kumvutia Bosi wangu, alikuwa mtu mgumu sana, kwa hivyo wakati mwingine ilikuwa vigumu kwangu kuelewana naye.

Kwa bahati wale ambao alioelewana naye ndio waliopatana nafasi ya kupandishwa daraja au kupata nyongeza ya mshahara, nilihisi kwamba hakuniona hata kidogo licha ya kazi nzuri nilizokuwa nafanya.

Niliamua kuwa mfanyakazi bora kwa kwenda kazini mapema, kufanya kazi zaidi na kufanya kazi hata masaa ya ziada lakini baada ya miezi michache, alimpandisha daraja mtu mwingine na kuniambia kuwa bado sijafika hatua hiyo.

Nilijisikia vibaya sana baada ya kusema hivyo, nilifikiria kuacha kazi kwa sababu nilikuwa nimefanya kazi katika kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka mitatu. Soma zaidi hapa.

Ujumbe kutoka Benki ya Dunia wakiongozwa na Bi. Gemma Todd wamefika ADEM Bagamoyo kufanya ufuatiliaji wa namna mafunzo ya Utawala Bora wa Elimu kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa yanayoendeshwa kwa Maafisa Elimu Kata nchini yanavyoendeshwa.

Wataalamu hao pia wamepata fursa ya kufanya kikao Mkakati na Mtendaji Mkuu Dkt. Maulid J. Maulid ambapo wamejadiliana mambo muhimu kuhusu namna ADEM inavyoweza kunufaika na miradi kutoka Benki ya Dunia hususani uwezeshwaji katika eneo la Kuimarisha Miundombinu ya Mifumo ya TEHAMA itakayosaidia kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa viongozi mbalimbali wa elimu nchini.

Vilevile, Wataalamu hao wamepata fursa ya kuzungumza na washiriki wa mafunzo hayo wapatao 246 kutoka Mkoa wa Iringa na Singida na kuwasisitiza kuhusu umuhimu wa kufanya usimamizi fanisi wa shughuli za elimu katika maeneo yao ili kufanikisha malengo ya programu ya BOOST ya kuboresha utoaji elimu ya Awali na Msingi nchini.