Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya Taifa Gesi imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi na salama ya gesi, sambamba na kuhamasisha usalama mahali pa kazi katika maadhimisho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani.

Akizungumza katika viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema, Njombe, Mtaalamu wa Masuala ya Afya, Mazingira, Usalama na Ulinzi Mahali pa Kazi kutoka Taifa Gesi, Aurelius Marcus Mdemu, alisema kampuni hiyo imeshiriki maadhimisho hayo yanayoanza Aprili 24 hadi 29, 2026 kwa lengo la kutoa elimu kwa wateja na jamii kwa ujumla.

 
Alisema kupitia banda lao, wanaonesha vifaa mbalimbali vinavyotumika kazini ili kuimarisha usalama wa wafanyakazi, pamoja na kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya gesi na faida zake. Aidha, alieleza kuwa wanajitahidi kuondoa hofu na dhana potofu zilizopo miongoni mwa watumiaji wa gesi.

“Tunawaonesha wananchi namna Taifa Gesi inavyoweka kipaumbele kwenye usalama wa wafanyakazi, ikiwa ni pamoja na matumizi ya vifaa kinga vinavyotakiwa kutumika muda wote wakiwa kazini,” alisema Mdemu.



 

Kwa upande wake, Afisa Masoko wa Chapa wa Taifa Gesi, Santina Ngaponda, alisema maonyesho hayo yameandaliwa na OSHA, yalianza Aprili 24 na yanatarajiwa kufikia kilele chake Aprili 29 mwaka huu.

Ngaponda aliwahimiza wakazi wa Njombe na maeneo ya jirani kutembelea banda la Taifa Gesi ili kupata elimu kutoka kwa wataalamu wa usalama, kujifunza matumizi sahihi ya gesi, pamoja na kuona vifaa vya usalama vinavyotumika kazini na umuhimu wake.
 

Aidha, aliongeza kuwa kampuni hiyo inatoa punguzo maalum la bei ya gesi na vifaa vyake, pamoja na zawadi mbalimbali kwa wateja watakaotembelea banda hilo.
 

Naye Meneja Mauzo wa Kanda ya Nyasa wa Taifa Gesi, Arnold Salewa, alisema wanaendelea kutumia maonyesho hayo kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya nishati safi pamoja na kuuza bidhaa zao kwa bei ya promosheni.

Alisema kanda hiyo inajumuisha mikoa ya Njombe, Iringa na Ruvuma, na kwamba pia wanatoa fursa kwa wananchi wanaotaka kuwa mawakala wao, kwa kuwapatia elimu ya biashara na usimamizi salama wa mitungi ya gesi.

Salewa alisisitiza kuwa Taifa Gesi ipo mstari wa mbele kuhakikisha kaya, migahawa na taasisi mbalimbali zinaanza kutumia nishati safi ya kupikia kwa gharama nafuu, ili kupunguza athari za matumizi ya mkaa na kuni kwa mazingira na afya za Watanzania.

Aliongeza kuwa mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa, huku Taifa Gesi ikiendelea kuwa chaguo sahihi kwa watumiaji wengi nchini.







 

Timu ya Wachezaji wa Karat a upande wa Kike na kiume zimeshiriki Mashindano ya mchezo wa Karata leo Aprili 25, 2026 katika viwanja vya Sabasaba mkoani Njombe.

Upande wa kike mshiriki Godlove Kyangala alichuana vikali na Timu ya Maliasili na kujinyakulia pointi nne (4) baada ya kumfunga Maliasili mzunguko yote miwili.

Mzunguko wa pili TCDC ilicheza na Wizara ya Madini na kupata pointi mbili (2) kwa mzunguko wa kwanza na mzunguko wa pili Timu zote mbili zilitoa sare ya mbilimbili.

Mzunguko wa tatu TCDC ilicheza na Uchukuzi na matokeo kuwa sare,ambapo kwa mzunguko wa nne TCDC ilipoteza pointi nne kwa kufungwa na timu ya IRDT na mzunguko wa tano na mwisho TCDC ilipoteza pointi nne dhidi Uwekezaji.

Kwa upande wa timu ya Karata ya kiume mshiriki alikuwa ni Zawadi Joseph ambapo mzunguko wa kwanza alicheza na Uchukuzi na matokeo kuwa sare ya mbili kwa mbili, mzunguko wa pili matokea pia yalikuwa sare Kati ya TCDC na Uwekezaji, mzunguko wa tatu kati ya TCDC na mzunguko wa tatu TCDC ilitoka sare tena dhidi ya TAKUKURU.

Mzunguko wa nne, TCDC ilipoteza pointi tatu dhidi ya Wizara ya Maji na kupoteza tena pointi tatu kwenye mchezo wake dhidi ya Ulinzi katika mzunguko wa tano.Katika mzunguko wa sita na wa mwisho Dodoma Jiji ilijinyakulia pointi nne kwa sifuri kwa TCDC.

Kwa matokea hayo TCDC Sports Club upande wa Karata Timu zote mbili hazikufanikiwa kuvuka hatua za makundi 16 bora katika michezo hiyo ya Meimosi.

Hapo Kesho Aprili 26, 2026, Jackson Mkoloweko na Grace Mnare wanatarajia kushiriki mchezo wa Bao utakaochezwa saa 2:30 asubuhi katka viwanja vya Sabasaba mkoani humo.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imeshiriki kikamilifu katika Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo (JWK) uliofanyika katika ukumbi wa soko la Kariakoo, jijini Dar es Salaam.
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imepokea vifaa vya kisasa vya uchunguzi wa kimaabara kutoka Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC), ikiwa ni pongezi baada ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika udhibiti wa dawa za kulevya nchini.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Ashatu Kijaji (Mb), akiwa katikati katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Hoteli ya Manyara’s Secret, iliyopo ndani ya Pori Tengefu la Mto wa Mbu, Wilaya ya Monduli, Mkoani Arusha.

Chama cha Wafanyakazi Serikali za Mitaa (TALGWU), tawi la RUWASA, kimefanya mkutano mkuu wa uchaguzi wa viongozi wapya ambapo Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Mhandisi Rashid Abdallah, amefanikiwa kutetea nafasi yake ya uenyekiti.

Uchaguzi huo ulifanyika Aprili 24, 2026 jijini Dodoma, katika mazingira ya uwazi na ushirikishwaji mpana wa wanachama, waliotekeleza haki yao ya kidemokrasia kwa kuchagua viongozi watakaoongoza tawi hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Katika uchaguzi huo, viongozi waliochaguliwa ni pamoja na Mhandisi Rashid Abdallah (Mwenyekiti wa Tawi), Ibrahim Fungo (Katibu wa Tawi), Tumaini Gwatalile (Mwenyekiti wa Makundi Maalum – Wanawake), Ashura Nkunya (Katibu wa Makundi Maalum – Wanawake), Victoria Charles (Mjumbe wa Makundi Maalum – Vijana), na Adam Suleiman (Mjumbe wa Makundi Maalum – Watu wenye Ulemavu).

Uongozi huo mpya unatarajiwa kuimarisha mshikamano miongoni mwa wanachama, kulinda na kutetea maslahi yao, pamoja na kuendeleza maendeleo ya chama katika tawi la RUWASA.








NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI imewahimiza wawekezaji wazawa kuchangamkia fursa zilizopo katika sekta ya viwanda, ikisisitiza kuwa imeendelea kuboresha na kurahisisha mazingira ya biashara ili kuongeza uwekezaji wa ndani.

Na Augusta Njoji

Timu ya wataalamu wa afya kutoka Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni imeanza rasmi mpango wa utoaji elimu kwa jamii ili kuimarisha kinga dhidi ya magonjwa na kuboresha ustawi wa wananchi.

Utoaji wa elimu hiyo imejikita katika afua za kuzuia malaria, lishe bora, bima ya afya kwa wote pamoja na huduma za mama na mtoto, ikiwa ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha jamii inakuwa na afya bora.

Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Ofisa Afya wa Halmashauri na Mratibu wa Elimu ya Afya kwa Umma, Jonas Mkondya, amesema wamejipanga kutembelea kila mtaa katika kata zote 12 za Halmashauri ya Mji Handeni ili kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwapatia elimu sahihi ya afya.

Ameeleza kuwa elimu hiyo itasaidia kuongeza uelewa kwa wananchi juu ya namna ya kujikinga na magonjwa, kuboresha lishe pamoja na umuhimu wa kujiunga na bima ya afya kwa wote ili kupata huduma kwa urahisi.

Kata zitakazofikiwa katika ziara hiyo ya wataalamu wa afya ni Konje, Mabanda, Kwenjugo, Malezi, Chanika, Mlimani, Mdoe, Vibaoni, Kwediyamba, Kideleko, Msasa na Kwamagome.

Timu ya Mpira wa miguu TCDC Sports Club imeonyeshana ubabe na Timu ya Mpira wa miguu ya Benki Kuu ya Tanzania (BOT) baada ya kutoka sare ya goli mbili kwa mbili katika mechi ya kirafiki iliyochezwa leo Aprili 24, 2026 katika viwanja vya Chai mkoani Njombe.

Hapo Aprili 22, 2026 TCDC Sports Club ilikubali kipigo cha bao moja bila 1- 0 kutoka Timu ya Mpira wa miguu ya TANWART katika mechi ya kirafiki iliyochezwa viwanja vya Kibena mkoani humo.

TCDC Sports Club inaendelea kushiriki Michezo ya kirafiki mkoani humo baada ya kushindwa kuvuka hatua za makundi kwenye Mashindando ya Michezo ya Meimosi inayoendelea mkoani humo.

 

Katika kuelekea Kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani ( Meimosi) ambayo kitaifa inafanyika mkoani Njombe, Timu ya Pooltable ya TCDC Sports Club imeshiriki mashindando ya mchezo huo Aprili 23, 2026 ndani ya African Club mjini humo.

Mchezaji Mbasso John ameiwakilisha TCDC Sports Club katika mchezo huo huku akishinda mechi ya kwanza kati ya TCDC na Ulinzi na ,mechi ya pili akicheza na Arusha DC na kutoka moja moja na kupoteza mchezo wa mwisho baada ya kufungwa na timu ya Mahakama.

Kwa hatua hiyo TCDC Sports Club haijafanikiwa kuingia nusu fainali katika mchezo wa Pooltable katika Mashindando ya Michezo ya Meimosi.

Wanamichezo wa TCDC Sports Club wameshiriki mashindano ya riadha (mbio) katika Michezo ya kitaifa Meimosi inayoendelea mkoani Njombe.

Wachezaji walioshiririki mbio hizo ni Mbaso John aliyekimbia Mita 100 na kuibuka mshindi wa tatu (3) katika round ya kwanza, na baadae kupoteza nafasi ya ushindi katika hatua ya nusu fainali.

Mchezaji mwingine ni William Valentine aliyeshiriki riadha mbio za Mita 800 na kutofaninikiwa kupata ushindi baada ya kuzidiwa na wanariadha kutoka Ofisi ya Rais - TAMISEMI na Wizara ya Mambo ya ndani.

Kwa upande wake Noel Steven ambaye pia ni Mwenyekiti wa TCDC Sports Club ameshiriki mchezo wa Draft ambapo kwa mzunguko wa kwanza TCDC Sports Club ilishinda mechi mbili na mzunguko wa pili kupata draw na hivyo kutofanikiwa kuvuka hatua za makundi baada ya kuzidiwa kete na TRA na Wizara ya Kilimo.

Michezo hiyo yote imechezwa Aprili 21, 2026 katika viwanja vya Njombe Sekondari na Viwanja vya sabasaba (77) mkoani humo.