Na Denis Chambi ,Tanga


SPIKA wa baraza la wawakilishi Zanzibar Zuberi Maulidi ameawataka watanzania kuendelea kuenzi na kudumisha tunu ya muungano  kati ya Tanganyika na Zanzibar iliyoasisiwa miaka 61 iliyopita kwa kuhakikisha kuwa  amani na umoja vinaendelea kutawala kwa kuweka maslahi ya Taifa mbele.

Spika Maulidi ametoa wito huo mkoani Tanga  katika maadhimisho ya muungano  ambayo hufanyika kila mwaka ifikapo Aprili 26 ambayo  mwaka huu yamebebwa na kauli mbiu isemayo ‘Muungano  wetu  ni dhamana heshima na tunu ya taifa shiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 akisistiza watanzania wenye sifa za kupiga kura  kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwa upande wa udiwani ubunge na kiti cha Rais.

Adha ameataka watanzanai waliopewa dhamana ya kusimamaia sekta mbalimbali hapa nchini kuhakikisha kuwa wanatekeleza vyema  majukumu yao  ikiwa ni pamoja na kusimamaia maono ya serikali kawenye miradi ya maendeleo.



 “Watanzania wenzangu tuendelee kuunga mkono maono ya viongozi wetu katika kuijenga nchi yetu  kupitia sekta mbalimbali ikiwemo  afya , maji barabara ,mawasiliano na biashara kwa kuwa tuko kwenye kilele cha maadhimish ya miaka 61ya muungano wetu niwakumbushe baadhi ya mambo ya msingi  yaliyofanya muungano wetu huu udumu  ikiwa ni pamoja  na dhamira ya dhati ya viongozi wetu waasisi kutokana na undugu wa kihistoria” amesema Maulid.

 “kauli mbuiMuungano wetu ni dhamana heshima na tunu ya taifa shiriki uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa kauli mbiu hiyo watanzania tumebarikiwa dhamana ya ya muungano wetu waibebe vizuyri dhamana hiyo kwa sababu watanzania wanaheshima kubwa kutokana na muungano mhuo ,na hivyo heshima hiyo ni vema tuendelee kuidumisha tuilinde na hatimaye kujitokeza kwa wingi kujitokeza kuchagua viongozi wetu kwa amani na utulivu kwa maana ndio njia kushiriki kwenye uchaguzi mkuu’ameongeza

Awali akizungumza mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt. Batilda Buriani tangu kuasisisiwa kwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar kupitia awamu zote ni mambo mengi ya kimaendeleo yamefanyika hususani kwenye awamu ya sita chini ya Rais wa Jamuhri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan.

 “Sisi ambao tumeukuta muungano wajibu wetu ni kuutuza , mambo mengi yamefanyika lakini   katika awamu hii ya sita chini ya Rais Samia Suuhu Hassan yamefanyika mengi zaidi ikiwemo ucumi kuimarika kinachotakiwa ni kuhakikisha kwamba  tunakwenda pamoja tukitanguliza mbele maslahi ya muungano wa nchhi hizi mbili  tunaomba sana amani iendelee kutwala” alisema Dkt. Buriani.

Akizungumza kwa niaba ya wabunge wa mkoa wa Tanga amabaye ni naibu waziri wa maliasili na utalii Datan Kitandula amepongeza juhudi zinazoendelea kufanywa na Rais Wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt SAmia Suluhu Hassan kupitia sekta mbalimbali ikiwmo afya ,elimu, miundombinu ambapo mkoa huo umenufaika kwa miradi mbalimbali ikiwemo ya kimkakati.

“Kwa niaba ya wabunge wa mkoa wa Tanga tunampongeza  sana  Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika muda ambao tumekuwa wawakilishi  wa wananchi hatukuwahi kuona maendeleo makubwa kama haya ya kipindi cha awamu ya  sita anayoiongoza” amesema Kitandula

Share To:
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: