Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka watanzania kujenga Taifa lenye Mshikamano, Amani na Umoja  kama ambavyo Muasisi wa Taifa Mwalimu JK, Nyerere alivyofanya katika kuwajenga watanzania.

Mhe. Biteko ameyasema hayo leo alipokuwa akifungua Kongamano la kumbukizi la kuzaliwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere lililofanyika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), katika ukumbi wa Utamaduni kampasi ya Kivukoni, jijini Dar es Salaam.

Mhe. Biteko amesema kumbukizi ya kongamano  Hilo linatoa fursa kwa Watanzania kukutana na kutafakari kwa  pamoja katika kujenga Taifa lenye mshikamano ambapo Baba wa Taifa alisisitiza misingi ya kuunganisha Makabila yote bila kujali kuangalia kwa kutuunganisha makabila yote bila kujali  dini,  na rangi ya mtu na kuwa kitu kimoja kwa lengo la kuleta Maendeleo katika.

Mhe. Biteko  amewataka vijana wa kitanzania kufanya tafakuri ya mambo ambayo Hayati Baba wa Taifa Mwalimu JK. Nyerere aliyaamini na kuyaishi kwa kujifunza kupitia makongamano ya aina hii ili kudumisha Amani, Upendo na Umoja wa kitaifa. 

Akimkaribisha Mgeni rasmi, Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara na Mwenyekiti wa bodi ya MNMA  Mhe. Stephen Wasira amesema Mwalimu Nyerere amewaunganisha Watanzania wote bila kujali dini wala kabila na kuwa kitu kimoja pia ameliacha Taifa likiwa na Amani  hivyo Amani hiyo  inatakiwa kulindwa  kwa nguvu na kutoruhusu watu ama kikundi chochote kuvuruga Amani  aliyotuachia Muasisi  wa Taifa Mwalimu JK. Nyerere.

Kwa upande wake  Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Prof. Haruni  Mapesa amesema lengo la Kongamano la Kumbukizi ya kuzaliwa Mwalimu JK.Nyerere ni kuyaenzi, kutafakari na kuyazungumzia kwa pamoja  juu ya Fikra, Mawazo na Itikadi zake hasa kupitia mada kuu isemayo Maono ya Baba wa Taifa Mwalimu JK. Nyerere katika Elimu, Uwekezaji, na Ujenzi wa Taifa lenye Amani kwa Maendeleo ya Watu.

Prof. Mapesa ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa Kukipatia Ruzuku ambazo zinasaidia katika Kutekeleza Miradi mbalimbali ya Maendeleo ya Chuo.

Kongamano la kumbukizi la kuzaliwa Baba wa Taifa Mwalimu JK Nyerere huandaliwa na Chuo kila mwaka kwa lengo la kuenzi na kutafakari Falsafa na Maono ya Baba wa Taifa.


Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano na Masoko

CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE


11.04.2025

Share To:

Post A Comment: