Na Oscar Assenga,MUHEZA.
HALMASHAURI ya wilaya ya Muheza Mkoani Tanga imesema kwamba itaendelea kuwaunga mkono madiwani ambao watakaoanzisha Ligi mbalimbali katika maeneo yao kwa lengo la kuhamasisha michezo na kufungua fursa za ajira kupitia sekta hiyo.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Issa Msumari wakati Fainali ya Ligi ya Erasto Cup ambayo imeanzishwa na Diwani wa Kata ya Tongwe Erasto Mhina ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri kwa lengo la kuhamasisha vijana kushiriki kwenye michezo.
Msumari ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira wilayani Muheza alimpongeza Diwani huyo kwa kuonyesha udhubutu na kupambana kuhakikisha anawapelekea burudani vijana wa Kata hiyo.
Katika mchezo huo wa fainali timu ya Mngeza B iliibuka na ushindi wa penati 5-4 dhidi ya Kwevumo FC katika mchezo ambao ulikuwa na upinzani mkubwa baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1 katika dakika 90 mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Pongwe kata ya Tongwe wilayani Muheza.
“Kwa wastani ligi hii imeongeza uchangamfu mkubwa na vijiji 6 na vitongoji 27 kuna badhi ya vijana walikuwa hawatambuani na ligi hiyo hivyo uwepo wake umekuwa chachu ya kuwaleta vijana pamoja na kufahamiana na inakuwa rahisi kuhamasisha mambo ya kijamii”Alisema
Aidha alisema ushiriki wa watu unakuwa ni mkubwa sana ambapo wilaya hiyo wanaunga mkono michezo kwa sababu inatengeneza ajira na kuondoa tatizo la vijana kukaa mtaani bila kazi ya kufanya hivyo wanaipa kipaumbele kama ya vijana watacheza na kutokea kwenye ligi mbalimbali watatengeneza vijana wengi ambao wataitangaza wilaya hiyo kupitia soka.
“Tutaendelea kuunga mkono michezo kwa sababu kupitia huko vijan a wanaweze kutengeneza pesa kama ilivyo kwa vijana wengine waliotokea wilaya ya Muheza Mzize na Semtawa na nieleze kwamba diwani ambayo ataanzisha michezo tutamuunga mkono kutokana na kwamba kupitia michezo inaweza kuwasaidia kuweza kujikwamua kiuchumi wao na jamii “Alisema
Post A Comment: