Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kundi la waasi la M23 wanatazamiwa kufanya mazungumzo ya kwanza ya moja kwa moja leo mjini Doha, Qatar, hatua muhimu katika mchakato wa kuhitimisha mzozo mkongwe mashariki mwa DRC unaoendela kwa miongo kadhaa.


Mazungumzo haya yanakuja wakati ambapo hali ya kibinadamu katika maeneo ya mashariki mwa Kongo inazidi kuwa mbaya, huku maelfu wakipoteza maisha na zaidi ya watu milioni moja kulazimika kuyakimbia makazi yao tangu mapigano kushika kasi mwanzoni mwa mwaka huu.


DRC, Umoja wa Mataifa na jumuiya za kikanda zinaishutumu Rwanda kwa kuunga mkono M23 kwa kuwapatia msaada wa kijeshi na silaha, tuhuma ambazo Rwanda imekuwa ikikanusha vikali.


Wakati wa shughuli ya kitaifa ya kumbukumbu ya mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994, Rais Paul Kagame hakuzitaja nchi moja kwa moja lakini alisisitiza kuwa matalfa hayo yanapaswa kuyatatua matatizo yao na kumwacha yeye ashughulkie ya kwake.


Kwa muda mrefu, jitihada za kidiplomasia zimesuasua. Mwaka jana, mazungumzo ya amani yaliyosimamiwa na Angola yalivunjika baada

ya Rwanda kushinikiza mazungumzo ya moja kwa moja kati ya serikali ya DRC na kundi la M23.


Siku moja baada ya M23 kutangaza kujiondoa kwenye mazungumzo hayo, Rais Felix Tshisekedi wa DRC na Rais Paul Kagame wa Rwanda walikutana ana kwa ana nchini Qatar kwa mara ya kwanza, mpatanishi akiwa ni Amir wa Qatar. 


Mazungumzo hayo yalichochea mwamko mpya wa kidiplomasia, na hivyo kufanikisha mashauriano yanayoanza rasmi leo.

Share To:

OKULY BLOG

Post A Comment: