Wanafunzi na Watoto wanaolelewa katika kituo cha kulea watoto wanaotoka kwenye mazingira hatarishi wakiwa katika eneo la bustani kwa ajili ya kupata elimu juu ya kilimo cha Mboga kutoka kwa Wanawake watafiti kutoka taasisi ya kimataifa ya utafiti wa Mboga Duniani "World Vegetable Center ya jijini Arusha ambao waliwatembelea watoto hao .
Mtafiti  Bi. Inviolate Mosha kutoka taasisi ya kimataifa ya utafiti wa Mboga Dunia "World Vegetable Center",akiwafundisha watoto katika kituo cha kulea watoto cha Motonyoki kilichopo Olasiti jijini Arusha namna ya kuotesha mboga .
Mtafiti  Bi. Inviolate Mosha kutoka taasisi ya kimataifa ya utafiti wa Mboga Dunia "World Vegetable Center",akiwafundisha watoto katika kituo cha kulea watoto cha Motonyoki kilichopo Olasiti jijini Arusha namna ya kuotesha mboga ,zoezi hilo likishuhudiwa na Mkurugenzi wa taasisi hiyo Colleta Ndungulu (wa pili kutoka kulia) walioshika majembe.
Sehemu ya timu kutoka taasisi ya kimataifa ya utafiti wa Mboga Dunia "World Vegetable Center",wakishuhudia namna ambavyo watoto katika kituo cha kulea watoto wanaotoka kwenye mazingira hatarishi cha Motonyok kilichopo Olasiti jijini Arusha wakifundishwa juu ya uoteshaji wa mboga 
Mtafiti Leticia akiwa akirejesha tabasamu kwa mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo cha kulea watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi cha Motonyok walipofika kutoa elimu .
Sehemu ya timu kutoka taasisi ya kimataifa ya utafiti wa Mboga Dunia "World Vegetable Center",wakishuhudia namna ambavyo watoto katika kituo cha kulea watoto wanaotoka kwenye mazingira hatarishi cha Motonyok kilichopo Olasiti jijini Arusha wakifundishwa juu ya uoteshaji wa mboga .
Sehemu ya timu kutoka taasisi ya kimataifa ya utafiti wa Mboga Dunia "World Vegetable Center",wakiongozwa na Mkurugenzi wake Colleta Ndungulu wakijadiliana jambo wakati wa utoaji elimu kwa watoto wanaolelewa katika kituo cha kulea watoto wanaotoka kwenye mazingira hatarishi cha Motonyok kilichopo Olasiti jijini Arusha.
Mtafiti  Bi. Inviolate Mosha kutoka taasisi ya kimataifa ya utafiti wa Mboga Dunia "World Vegetable Center",akiwafundisha watoto katika kituo cha kulea watoto cha Motonyoki kilichopo Olasiti jijini Arusha namna ya kukinga mbegu baada ya kuzisia kwenye udongo .
Baadhi ya watoto katika kituo cha kulea watoto cha Motonyok kilichopo Olasiti jijini Arusha wakisoma vipeperushi vikionesha namna ambavyo kilimo cha Mboga kinafanyika .
Mtafiti Dkt Judith Hurbert kutoka taasisi ya kimataifa ya utafiti wa Mboga Dunia "World Vegetable Center",akiwafundisha watoto katika kituo cha kulea watoto cha Motonyoki kilichopo Olasiti jijini Arusha namna ya kukinga mbegu baada ya kuzisia kwenye udongo .
Mkurugenzi wa taasisi ya kimataifa ya utafiti wa Mboga "World Vegetable Center" Colleta Ndunguku akiotesha mti wa kumbukumbu katika kituo cha kituo cha kulea watoto cha Motonyok kilichopo Olasiti jijini Arusha 

Na Dixon Hussein .

Arusha – Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa vitendo, wanawake wa Taasisi ya Utafiti wa Mboga Duniani (World Vegetable Center) waliamua kupeleka elimu ya kilimo cha mboga kwa watoto wanaolelewa katika kituo cha Matonyok kilichopo kata ya Olasiti, jijini Arusha.

Badala ya sherehe za kawaida, wanawake hawa waliamua kutumia siku hiyo muhimu kuwapatia watoto ujuzi wa uandaaji wa shamba na uoteshaji wa mboga, ili kuwasaidia kupata lishe bora na kuboresha afya zao. Mbali na elimu hiyo, walitoa msaada wa mahitaji mbalimbali ikiwemo mchele, sukari, sabuni, na nguo, hatua iliyowafanya watoto hao kujihisi kupendwa na kuthaminiwa.

Mkurugenzi wa kituo cha Matonyok, Bi. Emmy Nicholaus Sitayo, alieleza kuwa kituo hicho kilianzishwa mwaka 2006 kwa lengo la kuwahifadhi na kuwalea watoto wanaoishi katika mazingira magumu, wakiwemo wale waliokumbwa na vitendo vya unyanyasaji kama vile ukatili wa kijinsia, kupigwa, na kunyimwa haki zao za msingi. Hadi sasa, kituo hicho kinahudumia watoto 58, kati yao 30 wakiwa wasichana na 28 wavulana.

“Tunashukuru ujio wa wanawake wa World Vegetable Center, si tu kwa msaada walioleta, bali kwa elimu ya kilimo cha mboga walichowapa watoto wetu. Kupitia maarifa haya, watoto wataweza kupata mboga kwa chakula chao cha kila siku na hatimaye kuwa na lishe bora inayosaidia kuimarisha kinga zao za mwili,” alisema Bi. Sitayo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mkurugenzi wa World Vegetable Center, Bi. Colleta Ndungulu, alisema kuwa wanawake wa taasisi hiyo waliguswa na hali ya watoto wa Matonyok na waliamua kushiriki kwa vitendo katika kuwapa ujuzi wa kujitegemea badala ya msaada wa muda mfupi.

“Tumeona ni muhimu kuwasaidia watoto hawa kwa kuwapa ujuzi wa kilimo cha mboga ili waweze kujitegemea na kupata lishe bora. Hii ni sehemu ya juhudi zetu za kuhakikisha kuwa jamii ina uelewa wa umuhimu wa mboga katika afya na lishe,” alisema Bi. Colleta.

Mbali na uandaaji wa shamba na upandaji wa mboga, watoto hao pia walifundishwa kuhusu makundi mbalimbali ya vyakula na umuhimu wa kula lishe kamili. Mtafiti wa World Vegetable Center, Bi. Inviolate Mosha na Dkt Judith Hurebert , aliwahimiza watoto hao kula mlo unaojumuisha vyakula vya aina zote, ikiwemo nafaka, mizizi, nyama, samaki, maharage, na matunda, ili kujenga miili yenye afya.

Watoto wa Matonyok walionyesha shukrani kwa fursa hiyo, wakisema kuwa elimu waliyopewa itawasaidia si tu katika kituo chao, bali pia katika maisha yao ya baadaye. “Sasa tunajua jinsi ya kupanda mboga na kuzitunza hadi kuvuna. Tutakuwa na chakula chetu wenyewe,” alisema mmoja wa watoto kwa furaha.

Hatua hii ya wanawake wa World Vegetable Center ni mfano wa jinsi taasisi na makundi mbalimbali yanaweza kushiriki kikamilifu katika kubadili maisha ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu. Kwa kutumia Siku ya Wanawake Duniani kwa vitendo, wameleta mwanga mpya kwa watoto wa Matonyok, wakiwa na matumaini ya maisha yenye afya bora na ustawi endelevu.

Share To:

Post A Comment: