Na Denis Chambi, Tanga.

MBUNGE wa Jimbo la Korogwe vijijini Timotheo Mnzava amechangia kiasi cha Shilingi lakini tano (500,000) kwaajili ya kuweka Malumalu  katika kanisa la la Kiinjili la Kilutheli Tanzania 'KKKT'  Makumba lililopo wilayani Korogwe ambalo bado ujenzi wake unaendelea ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa  hivi karibuni.

Mzava ambaye alishiriki Ibada katika kanisa hilo   January 5,2025 kabla ya kuanza ziara yake  na kuzungumza na wananchi kwenye mikutano ya hadhara  katika maeneo ya   Makumba , Mayuyu na Magoma amewapongeza waumini  ambao walianza ujenzi huo tangu awali mpaka hatua hiyo lilipofikia likiwa limeshaanza kutumika.

"Ujenzi wa kanisa hili mpaka kufika hapa maana yake kuna watu wametumia nguvu zao walijitoa kwa hali na mali kwa kazi hii naamini Mungu anendelea kuwabariki  na niwapongeze sana  kwa kazi kubwa ya Mungu ambayo waliiifanya"

"Nitawaunga mkono kwenye kazi hii ya  ujenzi, nimeambiwa unaoendelea  kazi inayofanyika sasa ni kuweka Malumalu na mimi nitachangia sehemu ya kazi hiyo ili niwe sehemu ya uboreshaji wa miundombinu ya kanisa hili kama sadaka yangu" alisema Mzava

Aidha pamoja na kazi zinazofanywa na kamati za ulinzi na usalama katika kuwahakikishia watanzania amani amewataka waumini wa kanisa hilo kuendelea kuliombea nchi amani hususani mwaka huu kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa  Madiwani , wabunge na Rais.

"Sote kwa ujumla tuendelee kusimama kwenye nafasi zetu  kuiombea sana nchi yetu  ili iendelee kuwa mahali salama  sisi kama watanzania  Mwenyezi Mungu ametupa neema katika nchi ambazo  zipo kwenye mazingira mazuri  ya utulivu na  amani, na utulivu huu si kwa sababu tu ya vyombo vya usalama bali wapo watu wa Mungu ambao wanatumia nafasi zao ili kuliombea amani nchi yetu  tuendelee kuliombea amani Taifa letu" alisema

Mchungaji wa kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania 'KKKT' Makumba, Richard  Mkufya amemshukuru Mbunge kwa mchango huo ambao utakwenda kumaliza sehemu ya uwekaji wa Tairizi ambao tayari wameshaanza  kuweka kwa mchango iliyokuwa ikitolewa na  waumini wa kanisa hilo .

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye shule ya msingi Makumba  Diwani wa kata ya hiyo  Idd  Shebila amesema pamoja na  jitihada zilizofanywa na Serikali katika kuwasogezea  karibu huduma  wananchi  bado kuna changamoto mbalimbali ikiwemo uchakavu wa jengo la mama na mtoto lililopo katika Zahanati ya Kijiji hicho

"Hii zahanati ya kijiji ambayo ndiyo kongwe katika wilaya yetu ya Korogwe lakini mvua inaonyesha bati linavuja  tunahitaji ukarabati kubwa kwenye zahanati hii  lakini pia Kuna uchakavu wa jengo la mama na mtoto tukuombe Mbunge wetu temnea na changamoto hii tupate ufumbuzi" alisema Shebila .

Akizungumza kwa niaba ya wananchi  mwenyekiti wa kijiji  Nikodemas Liondo  amemuomba Mbunge kuwasaidia kupatiwa uelewa wa kutosha kuhusu gharama za mama wajawazito wanapofika katika kituo cha afya Magoma ambapo hutakiwa kulipia shilingi lakini mbili (200,000).

"Wakina mama wajawazito wanapofika katika kituo cha afya Magoma kwaajili ya kujifungua  iliyokea kama wanatakiwa kujifungua kwa upasuaji anaambiwa ni lazima atoe shilingi lakini mbili tunaomba hili tupatiwe elimu ili tuweze kulifahamu zaidi"



Mmoja wa wananchi wa kata hiyo 

"Bado zipo changamoto kwenye baadhi yawas maeneo lakini kama viongozi wetu ni jukumu letu kusimamia kuona changamoto hizo zinaisha  ikiwemo changamoto ya ukosefu wa maji, miundombinu ya Zahanati na shule  ya Sekondari Mzava yapo mengi ya kusema ikiwemo Umeme bado hayo yote tunaendelea nao na tunaamini yote yatafanyika kabla hatujamaliza mwaka huu"

"Serikali imetoka fedha kwaajili ya ununuzi wa vifaa Tina na magari ya kubebea wagombea katika hospitali yetu ya Magoma  katika awamu hii tumepata gari tunaielekeza halmashauri gari hilo lielekezwa kwenye hospital ya Magoma"

Serikali ilikubali kutoa fedha kwaajili ya kujenga mabwawa na sisi watu wa Korogwe tutajenga mabwwaw mawili ikiwemo la Mayuyu ambalo lilihatobiiwa na mvua  tumekubaliana ufanyike usanifu mpya wa haraka 


Share To:

Post A Comment: