Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Tanga, Husna Sekiboko, ametoa msaada wa vitimwendo 10 vyenye thamani ya shilingi milioni 5 kwa wanafunzi wenye ulemavu katika shule tatu zilizopo Jijini Tanga.


Shule hizo ni pamoja na Shule ya Sekondari Tanga School, Hotern na Maweni Sekondari zote za jijini Tanga .

Msaada huu unalenga kuboresha usafiri wa wanafunzi hao na kusaidia katika mchakato wa kujifunza.

Sekiboko amesema kuwa msaada huo utawasaidia wanafunzi wenye ulemavu kuondokana na changamoto mbalimbali zilizokuwa zikiwakabiri.


Share To:

Post A Comment: