Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu  ameipongeza Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kwa shughuli za utafiti wa Wanyamapori ambazo zina tija katika  sekta ya uhifadhi na utalii  ambayo inachangia asilimia 17% ya pato la Taifa.

Akizungumza  jijini Arusha wakati wa kikao na Menejimenti ya TAWIRI, Bw. Mchechu  amesema Ofisi ya msajili wa Hazina  itaendelea kushauri vyema katika kuimarisha Mashirika ya Umma yaweze kujiendesha kwa tija.

“nawapongeza kwa utendaji mzuri, nitoe wito kuendelea kuwa wabunifu kutumia  rasimali mlizo nazo kujiendesha kwa ufanisi” amehimiza  Bw.Mchechu

Naye, Mkurugenzi Mkuu TAWIRI Dkt, Eblate Mjingo amesema TAWIRI ni taasisi ya kimkakati  ambayo mbali na kutokuonekana  ikizalisha  fedha moja kwa moja ina mchango  mkubwa katika mapato yatokanayo na utalii nchini ambapo takwimu na taarifa za tafiti ndizo zinazonadi utalii na kuimarisha uhifadhi

Share To:

Post A Comment: