Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga, Mhandisi Juma Hamsini, amewataka wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi na wasimamizi wa vituo, kuzingatia falsafa ya 4R (Reconciliation- maridhiano, Reforms- mabadiliko, Resilience- ustahimilivu, na Rebuilding- kujenga upya) katika kufanya kazi zao.

Mhandisi Hamsini ameyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya siku moja ya Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi na wasimamizi wa vituo, yaliyofanyika leo, Jumatatu Septemba 30, 2024, katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Galanos Jijini Tanga.

Amesema Rais Samia Suluhu Hassan ni mtenda haki, na hivyo amewataka watendaji hao wa uchaguzi kutenda haki kwa kufuata miongozo, kanuni na sheria, ili uchaguzi uweze kufanyika vizuri na kuisha kwa usalama na amani. 

Kufanyika kwa mafunzo haya ni mfululizo wa matukio ya maandalizi kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 27\/11\/2024, ukiwa na kauli mbiu isemayo; "Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki uchaguzi".













Share To:

Post A Comment: