Mfanyakazi wa GPF ORGANICS LTD akiwa amebeba zao la Mdalasini tayari kwa hatua ya uchakataji.
Zoezi la uchakataji wa mazao ya viungo likiendelea  GPF ORGANICS LTD   kazi kubwa ya uchakataji inafanywa na wanawake ambapo asilimia 95 ya  waajiriwa wa  kampuni hiyo ni wanawake.
Zoezi la uchakataji wa mazao ya viungo likiendelea  GPF ORGANICS LTD   kazi kubwa ya uchakataji inafanywa na wanawake ambapo asilimia 95 ya  waajiriwa wa  kampuni hiyo ni wanawake.


Na Tukuswiga Mwaisumbe,Muheza Tanga


Ni habari zenye simulizi ya mafanikio kwa wanawake na wananchi wa shoroba ya Amani Nilo juu ya kilimo cha mazao ya viungo,  Bi Esther John Nzalia kutoka kijiji cha Antakae  kata ya Kwezitu ni mwanamke wa mfano ambaye analima na kuchajata mazao haya ya viungo.


Kabla ya ujio wa mradi wa USAID tuhifadhi maliasili anasema katika kijiji chao walilima na kuuza mazao kwa  mazoea yasiyo na tija, baada ya ujio wa mradi  wamepewa miche na elimu bure wameitumia  soko limepaa.


Serikali ni msimamizi wa umma dhidi ya wawekezaji katika Maendeleo ya kilimo,  Marekebisho ya kiuchumi yamesababisha kufunguka kwa sekta hiyo kwa uwekezaji binafsi katika uzalishaji na usindikaji  na masoko ya kilimo.


Ingawa Ushoroba huu una maeneo mazuri ya uzalishaji,  Bi Magreth David  ( GPF ORGANICS LTD) anasema uzalishaji na uuzaji wa mazao haya ya viungo bado ni wa chini, anasema  kuna ukuaji mkubwa wa mahitaji ya mazao ya viungo duniani ikiwa uzalishaji utakuwa na ubora hasa kilimo kisichotumia mbolea za viwandani.


Uwepo wa wadau hawa wa GPF ORGANICS LTD  ni fursa kwa wakazi wa shoroba hii ya Amani Nilo kiweza kupata soko la nje na kuweza kuuza mazao yao kwa bei nzuri na kulima mazao yenye ubora  unaozingatia kilimo HAI.

#USAID tuhifadhi maliasili

Share To:

mwangaza wa hbari

Post A Comment: