Mkurugenzi Msalala Rose Manumba ameawataka wataalam wa Halmashauri ya Msalala kuongeza weredi katika kuwatumikia wanachi ndani ya  maeneo yao ya kazi.

DED Manumba  ameyasema hayo alipofanya kikao kazi na wataalamu  kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambapo aliwasisitiza kuongeza juhudi na kuwa wabunifu katika kutekeleza majukumu yao katika maeneo yao ya kazi sambamba na kusimamia miradi inayo anzishwa kwa fedha za Serikali.

Sanjari na hilo pia aliwataka wataalamu hao kuwa mfano katika maeneo yao kwa kuhakikisha wanajiandikisha katika daftari la mpigakura  Serikali za Mitaa na kutoa elimu juu ya umuhimu wa kujiandikisha kwa jamii inayo wazunguka.








Share To:

Post A Comment: