Na Chedaiwe Msuya,WF


Wizara  ya Fedha imehitimisha utoaji wa mafunzo kuhusu Sheria ya Ununuzi kwa Umma  katika mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma.

Mafunzo hayo yaliyofanyika katika Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara ili yakilenga kuwapa uelewa kuhusu Sheria mpya ya Ununuzi wa Umma Sura namba 410. 

Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria kutoka Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta binafsi (PPPC), Bi. Flora Tenga alisema kuwa malengo ya mafunzo yalikuwa kuwaelimisha maofisa mipango na viongozi wote wanaohusika na ununuzi ili kufahamu fursa zilizopo katika Sheria hiyo na namna wanavyokwenda kuitekeleza. 

"Sheria ya Ubia kati Dekta ya Umma na Sekta Binafsi imetoa fursa mbalimbali katika miradi ya ubia ambapo kuna fursa na vivutio vingi vinavowavutia wawekezaji huku lengo lingine ni kuhusu Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, Sura Na. 103 iliyofanyiwa marekebisho mbalimbali na kutoa fusa mbalimbali katika miradi ya ubia," alisema Bi. Flora

Lifafanua kuwa kuna fursa nyingi, kuna vivutio vya kikodi na visivyo vya kikodi ambavyo vinavutia wawekezaji na kuna vivutio mbalimbali ambavyo wanataka kuwaelimisha wanaotekeleza miradi ya ubia.

Pia amewataka  wanaotekeleza miradi ya maendeleo, badala ya kusubiri  fedha za Serikali kutekeleza miradi hiyo  watumie Sheria hiyo kumwalika mbia mwekezaji aweze kuleta fedha za kutekeleza miradi hiyo ya maendeleo ikiwemo miradi midogo midogo inayotekelezwa kwenye Serikali za Mitaa

Vilevile alisema kuna Sheria ya Takwimu kwani maendeleo au mipango yoyote haiwezi kupatikana bila kujua takwimu zilizopo.

"Kwahiyo tuko hapa pia kuwaelimisha Maafisa Mipango na viongozi wengine namna ya kutumia Takwimu sahihi"alisema Bi. Flora

Naye Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Ununuzi wa Umma (PPRA) Kanda ya Kusini, Fenias Manasseh alisema kuwa wamelazimika kutoa mafunzo hayo kwa watumishi wa Serikali kutoka sekta mbalimbali ili kuwapatia elimu hiyo ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ili  waweze kujua fursa na mabadiliko yaliyopo kwenye Sheria hiyo ili waweze kufaidika nazo.

"Wengi wao hapa wanataka katika Taasisi Nunuzi wanaofanya kazi ya michakato ya ununuzi sasa kama hawaelewi mabadiliko yaliyojitokeza kwenye Sheria ya Ununuzi wa Umma wataendelea kuwa na mambo ya kizamani na kusababisha wahusika washindwe kufaidi hizi fursa nyingi mbalimbali za maendeleo,"alisema Bw.  Manasseh.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara, Bw. Abdillah Mfinanga alisema kuwa Wizara hiyo inaendesha mafunzo kwa watendaji wa Serikali waliopo katika ngazi za mikoa, halmashauri, majiji, miji na wilaya kufuatia kuwepo kwa changamoto mbalimbali zinazohusu utekelezaji wa Sheria hiyo.

Aidha mada zilizowasilishwa katika mafunzo hayo ni pomoja na utekelezaji wa Sheria ya Ununuzi wa Umma lenye lengo la kuwafahamisha watanzania juu ya fursa mbalimbali zinazopatikana katika sheria hiyo.

Share To:

Post A Comment: