Naibu Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi amehitimisha ziara yake ya siku tatu kutembelea watoa huduma za mawasiliano zilizopo Mkoa wa Dar es Salaam.

Amehitimisha ziara yake kwa kutembelea Kampuni ya TIGO ambapo amefurahishwa na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Kampuni hiyo sanjari na kutoa ajira kwa zaidi ya vijana mia tano.

Amesema uwekezaji uliofanywa unaendana na kasi ya dunia zaidi wakiungana na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuhakikisha huduma za mawasilano zinatolewa kwa ufanisi mkubwa.

Ziara yake Jijini Dar es Salaam imehusisha Kampuni ya Airtel, Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) na kuhitimisha Kampuni ya TIGO.









Share To:

Post A Comment: