Mbunge wa Tanga Mjini Ummy Mwalimu ameshiriki Ibada ya Misa ya kumuaga aliekuwa Diwani wa kata ya Masiwani Mhe Longson Njau iliyofanyika nyumbani kwake Mtaa wa Njombe Mpirani, Kata  ya Masiwani.

Akitoa salamu za pole kwa familia, ndugu, Waheshimiwa Madiwani wa Jiji la Tanga, Viongozi na wakazi wa Kata ya Masiwani kwa msiba huu mkubwa, Mhe Ummy alisema kuwa  alimtambua Mhe Njau kama diwani mpambanaji alietanguliza mbele maslahi ya wananchi wake wakati wote ikiwemo kuacha alama ya kudumu ya Ujenzi wa Shule ya Msingi Mbugani.

Hata hivyo amewahakikishia wananchi wa Masiwani kuwa katika nafasi yake ya Ubunge ataendelea kuwa karibu nao ili kuhakikisha mwendelezo wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kata hiyo hususani maboresho ya barabara.

Aidha Mhe Ummy ameiombea familia  ya marehemu kuwa  na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Ibada ya Misa ya leo ya kumuombea Mhe Njau ilihudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tanga, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Waheshimiwa Madiwani, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji pamoja na  wananchi wa Kata ya Masiwani na wana Tanga kwa ujumla.







Share To:

Post A Comment: