Msimamizi wa Uchaguzi  wa halmashauri ya Meru ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri  hiyo Mwl.Zainab Makwinya leo ametoa maelekezo ya kuongoza mchakato wa Uchaguzi kuanzia Uandikishaji wa Wapiga kura,uchukuaji na urejeshaji wa fomu kwa Mujibu wa sheria na kanuni zilizopo.

Maelekezo hayo yanatolewa  siku 62 kabla yasiku ya uchaguzi wa serikali za mitaa kufanyika kwa lengo la kuhakikisha kuwa utaratibu unafuatwa na kwamba  wapiga kura Pamoja na wagombea wanapata taarifa zote zinazohitajika kwa wakati.

Akizungumza na waandishi wa Habari  katika halmashauri hiyo Makwinya alisema kuwa fomu za kugombea zitatolewa na kutakiwa kurudishwa kuanzia tarehe moja hadi saba mwezi wa kumi na moja mwaka 2024, kwa msimamizi msaidizi  wa uchaguzi.

Aidha maelekezo haya pia yanafafanua hatua zitakazoongoza mchakato wa uchaguzi huo kuanzia uandikishaji wa wapiga kura,uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea,uteuzi wa wagombea,kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa  uwazi,haki na sheria kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.

Mwl.Zainabu alisema kuwa kwa mujibu wa kanuni ya 9 ya  kanuni za uchaguzi  wa mwenyekiti wa kijiji,wajumbe wa halmashauri ya kijiji na mwenyekiti wa kitongoji katika mamlaka za wilaya za mwaka 2024,tangazo la serikali GN namba 571,la tarehe 12/7/2024 na kanuni za uchaguzi katika mamlaka za miji midogo ya mwaka 2024 kupitia tangazo namba GN namba 572 ambazo zinatoa mwongozo mzima wa zoezi hilo la uchaguzi.

Alisema kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa utafanyika tarehe 27/11/2024,ambapo  zoezi la uandikishaji wa wapiga kura litafanyika kuanzia tarehe 11 hadi 21 mwaka 2024 katika vituo vilivyopoangwa.

Pia ametia wito kwa ajili ya wakazi wote wenye umri kuanzia miaka 18 na  kuendelea waliokidhi masharti ya kisheria wanaruhusiwa kushiriki katika uchaguzi huo,huku akiwataka  wakazi wenye umri kuanzia miaka 21 au zaidi kugombea nafasi ya uenyekiti wa Kijiji,ujumbe wa halmashauri ya Kijiji na enyekiti wa kitogoji wanaruhusiwa kuchua fomu za kugombea fomu katika ofisi ya msimamizi msaidizi wa uchaguzi.







Share To:

Post A Comment: