Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa (Mb) amewasili Mkoani  Shinyanga kwa ziara ya kikazi ambapo amepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme, leo tarehe 8 Disemba 2023.

Katika ziara hiyo, Waziri Bashungwa atakagua miundombinu ya barabara zilizoharibiwa na mvua kubwa za El-nino zinazoendelea kunyesha katika mkoa huo pamoja na maeneo mbalimbali  nchini.

Miundombinu hiyo iliyoharibiwa na mvua  ni pamoja na barabara ya Shinyanga - Old Shinyanga, barabara ya Old Shinyanga - Solwa, barabara ya Solwa - Kahama na miundombinu mingine ya barabara katika mkoa huo.

Share To:

Post A Comment: