Wadau wa sekta ya utalii, sekta ya ufugaji nyuki na mazao yatokanayo na Nyuki wametakiwa kujiandaa na mkutano mkubwa wa wadau wa ufugaji nyuki na wazalishaji wa mazao yatokanoyo na ufugaji nyuki utakao fanyika jijini Arusha nchini Tanzania mwaka 2027.

Haya yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dunstan Kitandula alipokuwa anatoa Salamu za Wizara kwenye Kongamano la Uwekezaji, Biashara na Utalii na Uzinduzi wa Mwongozo wa uwekezaji mkoa wa Tanga. 

Mhe. Kitandula alisema kwamba Kupitia mada mbalimbali zitakazowasilishwa katika kongamano  na maonesho yanayoendelea katika mabanda, anaamini kuwa wawekezaji wengi watavutiwa kuja kuwekeza katika Mkoa wa Tanga kwani fursa nyingi zitaelezwa hapa zikiwemo za sekta ya Utalii.

Mhe. Kitandula aliongeza kuwa mkoa una fursa za uwekezaji kwenye malazi (Hotel na Permanent Tented Camps) katika Hifadhi za Taifa Saadani na Mkomazi na Msitu wa Asili wa Amani (Amani Nature Forest Reserve), fursa za uwekezaji kwenye campsites katika mapango ya Amboni.

Pia aliongeza kuwa, kuna  fursa za uwekezaji katika usafiri na usafirishaji wa watalii kwa magari, fursa za uwekezaji katika mashamba ya miti, uwekezaji katika viwanda vya misitu, fursa za uwekezaji katika ufugaji nyuki na biashara ya mazao ya asali.

‘Kuna fursa za kiuchumi kwa kuendesha biashara za aina mbalimbali (vyakula, vinywaji na bidhaa za asili na za kitamaduni) na uwekezaji katika utalii wa fukwe na ikizingatiwa kuwa Mkoa wa Tanga unapakana na bahari ya Hindi’ alisema Mhe. Kitandula

Aidha Mhe. Kitandula alimsukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Balozi wetu namba moja katika Sekta ya Utalii nchini katika kutangaza vivutio vya Utalii pamoja na fursa za uwekezaji kupitia progamu yake ya Tanzania - The Royal Tour ambayo inaendelea kuitangaza nchi yetu katika masoko ya kimataifa ya utalii, pamoja na kuvutia uwekezaji katika sekta mbalimbali za kiuchumi nchini ikiwemo Utalii.

Share To:

Post A Comment: