Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Kampeni ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga imekemea tabia za baadhi ya wazazi na walezi kufanya ukatili kwa kuwanyanyasa watoto.

Wameyasema hayo baada ya kupokea taarifa na kuwatembelea watoto wanne aliotoroka nyumbani kwao Ushirombo Mkoani Geita na kukimbiania kwa babu yao kata ya Ibadakuli Mkoani  Shinyanga, kwa kile kinachoelezwa kutezwa na mama yao wa kambo.

Babu wa watoto hao, mzee Mwandu Nangi Malaba mkazi wa kitongoji cha Wiligwamabu kijiji na kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga amesema watoto hao wanne walitoroka nyumbani kwao toka mwezi Julai Mwaka huu 2023 ambapo mpaka sasa takribani miezi mitano hawajahudhuria shuleni.

Mzee Mwandu Malaba pamoja na mambo mengine ameiomba serikali kuingilia kati changamoto hiyo ili watoto waweze kupata haki yao ya elimu kwa kuhakikisha wanaendelea na masomo kwani mpaka sasa hakuna juhudi zozote zinazofanyika kwa wazazi.

“Naiomba serikali iingilie kati changamoto hii iweze kunisaidia wajukuu zangu waendelee na shule maana mimi sina mawasiliano na mama yao mzazi ila baba yao ambaye alishaoa mwanamke mwingine alipiga simu siku moja tu akiwaulizia kama watoto wamefika salama toka siku hiyo tukipiga namba yake haipatikani”.

“Mtoto wa kwanza anayekadiriwa kuwa na umri wa Miaka 15 alikuwa akisoma kidato cha kwanza shule ya Sekondari Businda Mkoani Geita, mtoto wa pili mwenye umri wa miaka 12 alikuwa akisoma darasa la sita (6) shule ya msingi Businda, mtoto wa tatu mwenye umri wa miaka 8 alikuwa akisoma darasa la kwanza shule ya msingi Businda pamoja na mtoto wa nne mwenye umri wa miaka 4 yeye alikuwa bado hajaanza kusoma”.amesema Mzee Mwandu

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga, ambaye ni Mwenyekiti idara ya maadili Bwana Solomon  Najulwa pamoja na katibu wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Bwana Daniel Kapaya wamelaani tabia zinazofanywa na baadhi ya wazazi na walezi katika jamii kuwafanyia ukatili watoto kwa kuwanyima haki zao za msingi ikiwemo haki ya elimu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha Wiligwamabu amekili kupokea taarifa za watoto hao toka Mwezi Julai Mwaka huu 2023.

Share To:

Misalaba

Post A Comment: