Na. Asila Twaha, Iringa


Timu ya wanawake kuvuta kamba TAMISEMI  imeanza vizuri kwa kuikaba koo Ras Kagera kwa   kuishinda kwa pointi  2- 0

katika Michezo ya Shirikisho ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) yalioanza leo, Mkoani Iringa.

 Ushindi huo umepatikana baada TAMISEMI  kupangwa kucheza na RAS Kagera  ambapo timu ya RAS Kagera haikuonekana uwanjani.

Kocha wa Timu ya Kuvuta Kamba TAMISEMI Chediel Masinga  amesema ushindi wao hauna shaka sababu umezingatiwa taratibu zote kutoka kwa uongozi kwa wao kushinda  pointi  2-0.

Ameeleza kuwa timu hiyo imeonyesha nidhamu, juhudi na ushirikiano wakati wote wa michezo na inaendelea   kufanya mazoezi.

Michezo ya Shirikisho ya Wizara na Idara za Serikali yameanza rasmi leo yanatarajiwa kufunguliwa kesho katika viwanja vya Samora Mkoani Iringa.

Share To:

Post A Comment: