Angela Msimbira,KONDOA

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),  anayeshungulikia Elimu, Dkt.Charles Msonde amesema  mwalimu ni mwezeshaji wa ujuzi ndani ya jamii hivyo wanawajibu wa kuhakikisha wanafundisha kwa umahiri.

Akifungua Septemba 29, 2023 mafunzo ya uongozi na usimamizi wa shule kwa walimu, Wakuu wa shule za msingi yaliyofanyika katika Halmashauri ya Mji Kondoa, amesema mwalimu ni kiungo muhimu katika  kuboresha elimu nchini na kuwahimiza kutimiza kikamilifu majukumu yao.

"Walimu wamepewa dhamana kubwa ya kuboresha  elimu katika taifa letu la Tanzania kwa kuwa  ndio anayeleta elimu bora katika taifa lake hivyo tunahitaji miundombinu, vifaa vya kufundishia lakini ukimchukua mwalimu bora ambaye ufundishaji unatoka kwenye moyo wake kwa ajili ya kusaidia watoto wa taifa lake hata akikaa kwenye mti akafundisha wanafunzi wataelewa,"amesema.

Amesema katika uwajibikaji wa mwalimu bora katika shule  ni uwepo wa Mwalimu mkuu bora mwenye maono ya kuleta mabadiliko katika shule yake na taifa kwa ujumla.

Amebainisha kuwa  walimu  wanajukumu kubwa la kumjenga mtoto katika maadili na ni wajibu wa walimu na maafisa maendeleo ya jamii kuhakikisha wanatoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa malezi ya watoto ili watoto waepukane na ukatili wa kijinsia.

"Hivyo mwalimu ni mlezi wa watoto kwa kuhakikisha   wanapata ujuzi, umahiri, stadi na mwelekeo wa kuwawezesha watoto hao kujiletea maendeleo yao binafsi, jamii na Taifa kwa ujumla, "amesema.

Ameeleza kuwa serikali imeandaa sera , mitaala  na miongozo mbalimbali ni jukumu la  Mwalimu kuhakikisha anaisimamia  kwa kuwa na watoto wenye umahiri, ujuzi na uelewa wanapatikana ndani ya jamii.

Aidha, amesema kuwa mwalimu akisimama katika nafasi yake ipasavyo  kwa  kuhakikisha  kila ngazi ya darasa kuna mabadiliko itasaidia  kuleta mapinduzi  ya elimu nchini



Share To:

Post A Comment: