Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Mhe.Raymond Mwangwala amewaagiza watumishi wa Idara ya Afya kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia taratibu na kanuni za kazi ili kuweza kuihudumia jamii inayowazunguka ipasavyo.

Amesema hayo alipokuwa akifungua  kikao cha kawaida cha utendaji  na tathimini  kichofanyika katika ukumbi wa Hospitali ya Wilaya ya Karatu ambapo amewaonya na kuwataka  watumishi kuwa na matamshi yenye lugha nzuri kwa wateja (jamii) pindi wanapowapokea na kuwahudumia huku akisisitiza madaktari na manesi (senior) wazoefu, kuwaelekeza vijana hao (Juniors) namna ya kufanya kazi na kuwasiliana na jamii wanayoihudumia.

“Kila mmoja afanye kazi kwa kufuata taratibu na kanuni kwa kuzingatia miiko ya kazi,na kuwa na  nidhamu kazini” alisema Mwangala

Pia amewagiza waganga wafawidhi  kuhakikisha wanasimamia ukusanyaji mapato katika vituo vya kutolea huduma  na Kupeleka bank Kwa usalama zaidi fedha zilizopatikana Ili baa

Share To:

Post A Comment: