Julieth Ngarabali  ,Kibaha


 Wajawazito na watoto wa umri wa miaka 0 mpaka nane katika kata ya Misugusugu  mjini Kibaha wameondokana na adha ya kusafiri  umbali wa zaidii ya km 20  kufuta huduma za afya  huko Mlandizi Kibaha Vijijini kufuatia kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa zahanati ya kisasa ya Saeni na kuanza kutoa huduma zote ikiwemo ya afya ya uzazi. 

Wajawazito hao ni miongoni mwa Wananchi takribani 14,000 wanaoishi kwenye  mitaa mitatu ya Saeni, Zogowale na Jonung"ha katika  kata ya Misugusugu mjini Kibaha  ambao awali walikabiliwa na changamoto ya kutembelea  umbali mrefu kufuata huduma za afya  

Akizindua kuanza huduma za afya katika zahanati ya Saeni ,Mbunge jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka  amesema kuanza kwa huduma hizo ni jitihada za  Wananchi wa maeneo hayo kujitolea nguvu zao,  yeye mwenyewe, halmashauri na Serikali 

Koka amesema wananchi walipochoshwa na adha ya kutembea umbali mrefu walitafuta eneo la ujenzi wa mradi huo  ambapo katika  kuwaunga mkono alichangia  sh. 6.5 Milioni kwa ajili ya kununua mifuko ya saruji ya kuanzia ujenzi huo na wadau wengine wakaunga jitihada hizo.

" Mnakumbuka wakati nilipoomba ridhaa ya kuwa Mbunge wenu mliniambia mna shida ya maji, barabara na zahanati niliwapigia magoti kuwaomba kuwa tutazitatua na kweli tumeshirikiana sisi ,halmashauri na Serikali ya CCM  leo tumekamilisha vyote maana ,zahanati ndio hii tumeifungua  ni mkombozi mkubwa sana hapa" amesema Koka

Koka alibainisha lengo lake kubwa ni kuwatumikia wananchi  hivyo atahakikisha anaendelea kushirikiana nao jimboni humo kwenye sekta zote ili waweze kuondokana na kero ambazo wamekuwa wakizipata.

Awali  mganga mfawidhi wa halmashauri ya mji Kibaha Peter Nsanya  amesema mradi wa Ujenzi  zahanati hiyo mpaka kukamilika umegharimu  sh. 181. milioni zilizotokana na nguvu za wananchi,mbunge huyo, halmashauri na Serikali kuu.

," mradi wa ujenzi huo utaweza kusaidia zaidi hasa kwa Upande kwa huduma za mama na mtoto ambao walikuwa wanapata shida ya kusafiri mbali kuzifuata huko  Mlandizi , hata hivyo bado upo upungufu wa  viti " amesema Dk. Nsanya

Aidha  Diwani wa kata ya Misugusugu Upendo Ngonyani amemshukuru Mbunge Koka kwa namna anavyoshirikiana na Wananchi kuzitatua changamoto zilizopo na piai kutekeleza ilani ya CCM  kwa vitendo 

Baadhi ya wakazi wa mitaa hiyo wameshukuru mradii huo kuanza kazi kwani itaongeza chachu ya wajawazito wengi kuanza kliniki mapema, kupata elimu ya lishe,kupata kinga ya maradhi mbalimbali ikiwemo saratan ya mlango wa uzazi na pia wengine kupata tiba kwa wakati

Share To:

mwangaza wa hbari

Post A Comment: