Katibu Mkuu wa Umoja wa  Wanamuziki Tanzania (TAMUFO), Stellah Joel.

..........................................................

Na Dotto Mwaibale, Arusha

UMOJA wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO) unatarajia kuwakutanisha wanamuziki, wananchi, viongozi na wadau mbalimbali  katika Tamasha kubwa litakalohusu mchango wa wanamuziki katika maendeleo ya nchi ambalo litafanyika kwa siku tatu jijini Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Katibu Mkuu wa TAMUFO Stella Joel alisema maandalizi yote yamekamilika na kuwa kwaya mbalimbali na wanamuziki binafsi watakuwepo kutoa burudani.

"Tamasha hilo litakuwa la siku tatu na litafanyika katika Makumbusho ya Taifa ya Elimu Viumbe Arusha jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa kuanzia Agosti 25 hadi Agosti 27, 2023," alisema Joel.

Alisema makundi ya kwaya na waimbaji binafsi watakuwepo kutoa burudani wakiongozwa na kwaya Kuu Habari Njema ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania|KKKT } na Kwaya ya Tangazeni ya kanisa hilo Unga Limited zote za jijini Arusha.

Alisema pia kutakuwa na bendi kutoka mikoa mbalimbali ambazo zitashiriki kutoa burudani kwenye tamasha hilo kubwa na la aina yake.

Alitaja kundi lingine ambalo litakuwepo ni wadau wa maendeleo ambapo pia kutakuwepo na fursa mbalimbali na kuwa kiingilio ni bure.

Joel alitumia nafasi hiyo kuwakaribisha wananchi na wadau mbalimbali wa muziki kufika kwenye tamasha hilo ambapo aliwataja baadhi ya wadau watakao kuwepo  kuwa ni pamoja na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Hifadhi |Dodoma ], Dkt.Noelia Myonga,  Agness Kanuty, Mwenyekiti wa Nokongo, Dkt. Lilian  Badi na Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa ya Elimu Viumbe Arusha, Dkt. Christina Ngereza.

Mlezi wa TAMUFO Dkt. Frank Richard alisema katika tamasha hilo Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) na COSOTA na TAMRISO watakuwepo kutoa elimu na usajili wa wanamuziki.

Mlezi wa TAMUFO Dkt. Frank Richard 
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Hifadhi |Dodoma ], Dkt.Noelia Myonga

 Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa ya Elimu Viumbe Arusha, Dkt. Christina Ngereza.

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: