RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan ameridhishwa na mabadiliko yanayoendelea Bohari ya Dawa ( MSD) na kuwataka waendeleee kuchapa kazi.

Rais Samia amesema hayo  Jumamosi Agosti 19, 2023 jijini Arusha wakati akifungua kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na taasisi za umma.

Rais Dk.Samia akiwa amemsimamisha Mkurugenzi wa MSD, Mavere Tukai alisema taasisi hiyo ni kati ya mashirika yaliyo badilika na matumaini yake itakwenda kufanya vizuri hasa katika mfumo wa  uuzaji wa Dawa Afrika kwa kuwa na soko kubwa hususani kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (SADC).


Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: