![]() |
Na Shamimu Nyaki - WUSM, Dodoma
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe,
Mohammed Mchengerwa amewaasa watanzania kulinda na kuhifadhi rasilimali
na kumbukumbu ambazo ni ushahidi wa Harakati za Ukombozi wa Bara la
Afrika katika maeneo waliyopo ambayo kumbukumbu hizo zinapatikana.
Katika
taarifa aliyoitoa kwa Vyombo vya Habari leo Mei 25, 2022 jijini
Dodoma, Mhe. Mchengerwa amesema Siku ya Afrika ambayo huazimishwa Mei
25 kila Mwaka,ni siku muhimu kwa waafrika wote ambapo kwa mwaka huu
imebebwa na Kauli Mbiu isemayo "Urithi wa Ukombozi, Fahari ya Afrika na
Kazi Iendelee".
"Kuthamini
utanzania wetu ni jambo la msingi na ndiyo kielelezo na sifa
iliyosababisha Umoja wa Afrika (AU) zamani (OAU) kuichagua Tanzania kuwa
Makao Makuu ya Kamati ya Ukombozi wa Bara la Afrika na kuipa hadhi ya
kuwa Mratibu wa Harakati za Ukombozi hadi nchi zote za Afrika zilipopata
Uhuru mwaka 1994" amefafanua Mhe.Mchengerwa.
Mhe.
Mchengerwa ameongeza kuwa, ni wajibu wa jamii ya waafrika kuenzi kwa
vitendo mashujaa wa Tanzania waliojitoa mhanga Kwa ajili ya Afrika chini
ya Uongozi wa Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.
Katika
kuadhimisha siku hiyo, watanzania wameaswa kutembelea Ofisi ya Programu
ya Urithi wa Ukombozi wa Afrika ili kujifunza na kuona ushahidi
waTanzania katika kuikomboa Afrika.
Post A Comment: