Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack ameongoza mazishi ya kaka
wa Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga, Mhe. Azza Hilal Hamad (CCM)
Abel Bulugu Kaheza (52) aliyefariki dunia siku ya Alhamis Agosti 22,2019
jijini Dar es salaam akisumbuliwa na kansa ya koo.
Mazishi hayo yamefanyika leo Jumatatu Agosti 26,2019 katika kijiji cha
Jomu kata ya Tinde wilaya ya Shinyanga ambapo mamia ya waombolezaji
wameshiriki mazishi hayo.
Akitoa salamu za pole na rambirambi,Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack amesema :
"Kwa niaba ya serikali na wakuu wote wa wilaya wapo hapa,Mhe.Azza
tunakupa pole sana,viongozi wote wa serikali wapo hapa kwa ajili ya
kukuunga mkono na kukupa pole kwa msiba huu mkubwa,tunajua wote
tumeguswa lakini hatuna namna,tungekuwa na uwezo tungeweza kusema
aendelee kubaki lakini kwa kuwa hatuna uwezo tumwachie Mungu",amesema
Telack.
"Namuomba mwenyezi Mungu awape subira katika wakati huu mgumu lakini
kikubwa tuendelee kumwombea marehemu kwa mwenyezi Mungu. Siku zote
tunasema,msiba uunganishe watu,lakini msiba usichonganishe
familia",ameongeza Telack.
Mhubiri katika ibada ya mazishi alikuwa Mchungaji wa Kanisa la AICT
Tinde William Shinyanga huku kiongozi wa ibada akiwa ni Nuhu Manoni
kutoka kanisa la AICT Tinde.
Abel Bulugu Kaheza alizaliwa Julai 1,1967 na amefariki dunia Agosti
22,2019 wakati akiendelea kupatiwa matibabu ya kansa ya koo katika
hospitali ya Lugalo jijini Dar es salaam.
ANGALIA PICHA
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab
Telack akimpa pole Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga, Mhe. Azza
Hilal Hamad (CCM) kwa kufiwa na kaka yake Abel Bulugu Kaheza leo
nyumbani kwake kijiji cha Jomu kata ya Tinde wilaya ya Shinyanga. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta Mboneko akiteta jambo na Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack nyumbani kwa Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga, Mhe. Azza Hilal Hamad (CCM) aliyefiwa na kaka yake Abel Bulugu Kaheza.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta
Mboneko akimpa pole Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga, Mhe. Azza
Hilal Hamad (CCM) kwa kufiwa na kaka yake Abel Bulugu Kaheza.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta Mboneko akiwapa pole wafiwa.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu,Mhe. Nyabaganga Talaba akiwapa pole wafiwa.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga,Mabala Mlolwa akimpa pole kwa kufiwa na kaka yake Abel Bulugu Kaheza.
Mbunge wa jimbo la Msalala,Mhe Ezekiel
akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack wakati wa
msiba wa Abel Bulugu Kaheza.
Viongozi mbalimbali wa Chama Cha
Mapinduzi mkoa wa Shinyanga wakiwa katika msiba wa Abel Bulugu Kaheza
leo nyumbani kwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal
Hamad.
Jeneza lililobeba Mwili wa marehemu Abel Bulugu Kaheza likitolewa ndani kwa ajili ya ibada na waombozaji kuaga mwili huo.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab
Telack na wakuu wa wilaya wakiwa wamesimama wakati mwili wa marehemu
Abel Bulugu ukitolewa ndani na kuwekwa nje kwa ajili ya ibada na
waombolezaji kuuaga.Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kahama, Mhe.
Anamringi Macha akifuatiwa na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta
Mboneko,wa kwanza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Kishapu, Mhe. Nyabaganga
Talaba.
Mchungaji wa Kanisa la AICT Tinde William Shinyanga akiendesha ibada ya mazishi ya marehemu Abel Bulugu Kaheza nyumbani
kwa Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad leo
katika kijiji cha Jomu kata ya Tinde wilaya ya Shinyanga.
Mchungaji wa Kanisa la AICT Tinde
William Shinyanga akiongoza ibada ya mazishi ya Abel Bulugu Kaheza
(ambaye ni kaka wa Mbunge Azza Hilal) leo nyumbani kwa Mbunge Azza Hilal
Hamad katika kijiji cha Jomu kata ya Tinde halmashauri ya wilaya ya
Shinyanga.
Kiongozi wa ibada ya mazishi ya Abel
Kaheza, Nuhu Manoni kutoka kanisa la AICT Tinde akizungumza wakati wa
ibada ya mazishi nyumbani kwa Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa
Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad leo katika kijiji cha Jomu kata ya Tinde
wilaya ya Shinyanga.
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa
Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad (mwenye kiremba cheusi katikati) akiwa
kwenye ibada ya mazishi ya kaka yake Abel Bulugu Kaheza.
Ndugu wa marehemu Abel Bulugu Kahiza wakiwa kwenye ibada ya mazishi ya marehemu Abel Bulugu Kaheza.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack akitoa salamu za pole na rambirambi kufuatia kifo cha Abel Bulugu Kaheza.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack akitoa salamu za pole na rambirambi kufuatia kifo cha Abel Bulugu Kaheza.
Mbunge wa jimbo la Msalala,Mhe Ezekiel akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya wabunge 9 wa mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga,Mhe. Mabala Mlolwa akitoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Abel Bulugu Kaheza.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab
Telack( watatu kutoka kushoto akiwa msibani. Wa kwanza kushoto ni Mkuu
wa wilaya ya Kahama, Mhe. Anamringi Macha akifuatiwa na Mkuu wa wilaya
ya Shinyanga,Mhe. Jasinta Mboneko,wa kwanza kulia ni Mkuu wa wilaya ya
Kishapu, Mhe. Nyabaganga Talaba.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack akiaga mwili wa marehemu Abel Bulugu Kaheza.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta Mboneko akiaga mwili wa marehemu Abel Bulugu Kaheza
MNEC Gaspar Kileo akiaga mwili wa marehemu Abel Bulugu Kaheza
Waombolezaji wakiendelea kuaga mwili wa marehemu Abel Bulugu Kaheza.
Waombolezaji wakiwa msibani.
Kwaya kutoka kanisa la AICT Tinde ikimsifu Mungu kwa nyimbo wakati wa ibada ya mazishi ya marehemu Abel Bulugu Kaheza.
Mazishi ya mwili wa marehemu Abel Bulugu Kaheza yakiendelea leo Tinde.
Ibada ya Mazishi ya mwili wa marehemu Abel Bulugu Kaheza ikiendelea.
Mchungaji wa Kanisa la AICT Tinde William Shinyanga akiweka mchanga katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Ibada wakati wa mazishi ya marehemu Abel Bulugu Kaheza ikiendelea.
Ndugu wakiweka mchanga katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Ndugu wakiweka mchanga katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Ndugu wakiweka mchanga katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Ndugu wakiweka mashada ya maua katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Ndugu wakiweka mashada ya maua katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Ndugu wakiweka mashada ya maua katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Ndugu wakiweka mashada ya maua katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Ndugu wakiweka mashada ya maua katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Ndugu wakiweka mashada ya maua katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Ndugu wakiweka mashada ya maua katika kaburi la marehemu Abel Bulugu Kaheza
Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi CCM mkoa
wa Shinyanga,Mhe. Abdalah Simba na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa
Shinyanga,Mhe. Mabala Mlolwa wakiweka shada la maua katika kaburi la
marehemu Abel Bulugu Kaheza
Mkuu wa wilaya ya Kahama, Mhe. Anamringi Macha akiweka shada la maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta
Mboneko akiweka shada la maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza kwa
niaba ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack.
Mbunge wa Jimbo la Solwa, Mhe. Ahmed Salum akiweka shada la maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga,Mhe. Hoja Mahiba akiweka shada la maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza.
Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya
Shinyanga wakiongozwa na mwenyekiti wa halmashauri hiyo Ngasa Mboje
wakiweka shada la maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB wakiweka shada la maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza.
Mwenyekiti wa CCM kata ya Tinde, akiweka shada la maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza.
Zoezi la uwekaji mashada ya maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza likiendelea.
Zoezi la uwekaji mashada ya maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza likiendelea.
Zoezi la uwekaji mashada ya maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza likiendelea.
Zoezi la uwekaji mashada ya maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza likiendelea.
Wakazi wa Tinde wakishuhudia mazishi ya marehemu Abel Bulugu Kaheza.
Mchungaji wa Kanisa la AICT Tinde William Shinyanga akiweka shada la maua katika kaburi la Abel Bulugu Kaheza.
Post A Comment: