Mkurugenzi wa kiwanda cha kutengeneza Gypsum cha  ST, GOBAIN LODHIA  kilichopo Kikatiti ,wilaya ya Arumeru mkoani Arusha,Sailesh Pandit  ametishia kukifunga  kutokana na kupanda Marà dufu kwa  gharama ya malighafi ya Makaa ya Mawe yanayotumika  kiwandani hapo.

Aidha ameiomba serikali kuangalia uwezekano Wa kuwapunguzia gharama za bidhaa hiyo ili waweze kujiendesha kwa faida tofauti na sasa ambapo kiwanda hicho kinajiendesha kwa hasara.

Pandit ameyasema hayo jana jmosi feb 10 wakati akizungumza na wafanyakazi wake baada ya wafanyakazi hao kudai nyongeza ya mshahara.

Amesema kuwa awali serikali ilikuwa  ikiwatoza asilimia 10 ya  thamani ya mzigo Wa Makaa ya Mawe lakini ghafla ilipandisha na kufikia asilimia 25 jambo linalopelekea kupata hasara ya zaidi ya sh, milioni 30 kila mwezi.

Amesema kuwa iwapo serikali haitasikia kilio chake atalazimika kusitisha uzalishaji hadi hapo hali itakapokuwa nzuri.
Amewasihi wafanyakazi wake ambao ni zaidi ya 1000 kuwa wavumilivu wakati akifanya mawasiliano na serikali.

  



Share To:

msumbanews

Post A Comment: