Kabla ya kuingia katika maisha ya ndoa, wale walengwa wanakuwa na mitazamo yao tofauti waliyojijengea lakini wanakuwa na picha fulani ya matokeo watakayoyapata baada ya kuingia kwenye maisha ya ndoa. Hivyo, mambo huwa ndivyo sivyo pale watu wanapokutana na mambo tofauti na kile walichotarajia kukikuta.
Kabla ya kuingia katika wito wowote kaa chini na tafakari mwenyewe unafaa kuingia katika maisha gani, kwa sababu siyo kila mtu ameitwa kuwa mwanandoa kuna aina nyingi za maisha ambayo unaweza kujichagulia kuishi. Kabla ya kuingia katika wito au maisha ya ndoa jichunguze kwanza je una fiti katika maisha ya ndoa kwa sababu wewe mwenye unajijua.
Rafiki, usiingie katika mahusiano ya ndoa kwa hisia, ingia katika maisha ya ndoa kwa kuongozwa na akili na ishi na mtu mwenye akili yaani mtu sahihi ndiyo utaweza kufurahia maisha ya ndoa.
Share To:

msumbanews

Post A Comment:

Back To Top