WAKAZI wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, wameiomba serikali  kupitia Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), kuweka matuta katika barabara ya Sanya Juu- Bomang’ombe, ili kuzuia ajali ambazo zimekuwa zikitokea na kusababisha watu kupoteza maisha.

WAKAZI wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, wameiomba serikali  kupitia Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), kuweka matuta katika barabara ya Sanya Juu- Bomang’ombe, ili kuzuia ajali ambazo zimekuwa zikitokea na kusababisha watu kupoteza maisha.

Wakazi hao wamesema barabara hiyo kwa muda mrefu imekuwa na ajali nyingi za watu kugongwa na magari na kupoteza maisha papo hapo na hakuna jitihada zozote ambazo zimekuwa zikichukuliwa na serikali kuzuia ajali hizo.

Mmoja wa wakazi wa Majengo Sanya Juu, Idrisa Mndeme, alisema serikali kupitia Tanroads inapaswa  kuwawekea matuta katika barabara hiyo kwenye maeneo ya kuanzia Standi Kuu ya Sanya hadi Fuka, kwa kuwa madereva wa magari wamekuwa wakiendesha kwa mwendo kasi bila kujali watembea kwa miguu.

“Ndani ya mwezi huu kuna ajali mbili zimetokea. Mtu mmoja aligongwa na gari na kupoteza maisha na mwingine ambaye ni mwendesha pikipiki aligongwa na gari na kufariki papo hapo,”alisema.

Yassin Kimaro kwa upande wake aliwatupia lawama madereva wenye magari makubwa kwa kuendesha kwa mwendokasi na mara nyingine hudharau alama za pundamilia kwa kupitisha magari bila kujali watu wanaovuka.

“Madereva wa magari huendesha magari kwa kasi mno, hali ambayo imekuwa ikichangia sana ajali ambazo zinaweza kuepukika iwapo matuta yangekuwa yamewekwa,”alisema.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Siha, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Onesmo Busweru, alikiri kuwapo kwa baadhi ya madereva ambao wamekuwa wakiendesha kwa kasi, hivyo kusababisha ajali ambazo zingeweza kuepukika

Kutokana na hali hiyo aliagiza Jeshi la Polisi kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani  kuweka kidhibiti mwendo (tochi) katika maeneo hayo ili kuwadhibiti madereva ambao wamekuwa akiendesha kwa kasi
Share To:

msumbanews

Post A Comment: