WAKATI Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa akipandishwa kizimbani jana, akidaiwa kuchoma nyumba aliyokuwa akiishi Katibu wa UVCCM Iringa, wabunge wengine kumi, wanasota kizimbani kwa kesi mbalimbali zinazowakabili.
Kesi za watunga sheria hao, zipo kwenye mahakama tofauti nchini, huku baadhi yao wakiwa na zaidi ya kesi moja kwenye mahakama tofauti.
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), ambaye kwa sasa anatibiwa nje ya nchi, anakabiliwa na kesi za uchochezi zaidi ya moja kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Naye Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), anakabiliwa na kesi ya uchochezi mkoani Arusha na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Chadema) naye anakabiliwa na kesi ya uchochezi ambayo kwa sasa mashahidi wa upande wa mashtaka wanatoa ushahidi wao.
Wabunge wengine wa Chadema, Peter Lijualikali, Mbunge wa Kilombero na Suzan Kiwanga wa Mlimba, wanakabiliwa na kesi ya uchochezi mkoani Morogoro.
Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema), anakabiliwa na kesi ya kumshambulia mwili Mbunge mwenzake wa Viti Maalumu, Juliana Shonza (CCM).
Wabunge wengine wa Chadema, Cecil Mwambe (Ndanda), Pascal Haonga (Mbozi) na Frank Mwakajoka (Tunduma) wote wanakabiliwa na kesi za uchochezi.
Naye Mbunge wa Donge, Sadifa Khamis Juma (CCM), anakabiliwa na kesi ya rushwa mkoani Dodoma.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: