Naibu waziri wa elimu sayansi na Teknolojia William Ole Nasha ameviagiza vyuo vya ufundi kote nchini kuondoa vikwazo na kutoa upendeleo maalum kwa wanafunzi wa kike wenye sifa wanaojiunga na elimu ya ufundi kwakuwa  idadi kubwa wanafunzi wa kike wanaichukia elimu ya ufundi kutokana na vikwazo vilivyopo kwenye vyuo hivyo dhidi yao.

Naibu waziri Ole Nasha ametoa kauli hiyo alipokuwa anazungumza na wahitimu wa fani mbalimbali za ufundi kwenye chuo cha ufundi Arusha ATC.

Kaimu mkuu wa chuo cha ufundi Arusha Dkt. Masud Senzia amesema chuo hicho kimetekeleza kwa vitendo adhima ya serikali ya viwanda kwani kimeanza kufanya majaribio ya kuzalisha umeme kwa njia ya maji.

Mkurugenzi wa elimu ya ufundi Thomas Katebalirwe akaelza mikakati ya serikali katika kuboresha elimu ya ufundi.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: