Watanzania wameombwa kujitokeza kwa wingi kufanya usahili kwenye kampuni ya Bravo job center ageny, ilikujipatia nafasi ya kwenda kufanya kazi nchini Saud Arabia.

Hayo yamesemwa leo na Mbunge wa Zamani wa Temeke ambae pia ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Abbas Mtemvu wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari jijini Dar es salaaam Leo.

Mtemvu amesema anamuunga mkono Rais Magufuli katika kuhakikisha wananchi wanapata ajira njema ,huku akitoa shukrani za Dhati  kwa Balozi Tanzania nchini Saud Arabia Mh Mgaza kwa kutoa ushirikiano wa hali ya Juu katika kufanikisha suala hilo.

“Tunazo nafasi 2000 Masezmen, na asistant sezmen,wapishi, Mainjinia,Madereva wa Magari Makubwa,Mainjinia wa Refregration and  air Condition,machenical,na oparetor wa Plastic Mashine kwa hiyo niwaambie tu watanzania kwamba Bravo inamuunga mkono Mh Rais Magufuli kuhakikisha watanzania wanapata ajira, na Al-marai Ni Kampuni kubwa sana inayotambulika kiserikali”Amesema Mh Mtemvu.

Kwa Upande wake Iddi Mawad ambae amepita katika usahili huo amewataka wananchi kujitokeza kufanya usahili nakusema kuwa katika kampuni hiyo hakuna udanganyifu wowote kama taarifa zuilizoenea mitaani.

Usahili huo unafanyika nyuma ya Uwanja wa Taifa (Shamba la bibi)Jijini Dar es salaam .
Share To:

msumbanews

Post A Comment: