DANSA 
maarufu Bongo, Moses Iyobo, amesema kuwa kuandika kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram kuwa amenyimwa penzi na mzazi mwenzie Aunt Ezekiel hajaona kama kuna tatizo ingawa aliandika kama utani.

Akizungumza na mwandishi wetu  Iyobo alisema kuwa yeye na Aunt ni watu ambao wanataniana sana japokuwa tayari ni wazazi kwa hiyo hata alipoandika juzikati Instagram, alikuwa kwenye kuendeleza utani japo mashabiki wao wameipokea vibaya.

“Unajua watu wanashindwa kuelewa lakini mimi na mama Cookie (Aunt) tunataniana sana kwa hiyo hata kuandika vile ni kumtania tu sasa watu hawakuelewa naona wametoa povu kweli,” alisema Iyobo.
Iyobo alikomenti kwenye video aliyoposti Aunt ikimuonesha akitembea akisindikiza na ujumbe wa neno ‘fresh’:

“Umeninyima penzi halafu uposti fresh?” alikomenti Iyobo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: