JESHI   la  polisi  mkoani  Iringa  linamshikilia mbunge  wa  jimbo la  Iringa mjini Mchungaji  Peter Msigwa kwa mahojiano kutokana na matukio ya  kiuharifu yanayotokea mjini Iringa .

Kamanda  wa  polisi  mkoa  wa  Iringa (RPC)  Julius Mjengi  ameuthibitishia  mtandao  huu  usiku huu  baada ya  kupigiwa  simu  kuhusiana na  kuzagaa kwa taarifa  za kukamatwa  kwa  mbunge Msigwa  katika  mitandao ya  kijamii .

Kamanda   huyo amesema  kuwa ni kweli hadi majira ya saa8.25  usiku  huu alikuwa akihojiwa  juu ya matukio ya uvunjwaji  wa  nyumba ya  aliyekuwa  diwani  wa kata ya Mwangata  kupitia  chadema aliyejiuzulu na kujiunga na CCM pamoja na tukio la  kuchomwa  moto  kwa  nyumba  aliyokuwa akiishi katibu  wa UVCCM Iringa mjini .

"  Bado  tunaendelea  kumhoji na  ni kweli  amekamatwa  tupo  naye tunaendelea  kumhoji "
Share To:

msumbanews

Post A Comment: