Kufuatia Tukio hilo Juma Nyosso alikamatwa na Polisi na Kupelekwa kituoni, Zipo taarifa zilizosema kuwa amelala kituoni (Polisi) lakini taarifa za Kuaminika ambazo Kocha Mkuu wa Kagera Sugar Meck Mexime ameiambia Msumbanews.co.tz Asubuhi ya Leo ni Kwamba Nyosso alitoka jana mara baada ya Kuandika Maelezo katika  Kituoni Polisi na leo mambo mengine Yataendelea.

Kanuni zinasemaje juu ya Tukio la Juma Nyosso? Hizi Hapa

Kanuni ya 37 Ya udhibiti wa Wachezaji inasema mchezaji atakayesababisha na kufanya vurugu za aina yoyote na mara baada ya mchezo kumalizika atafungiwa kati ya michezo mitatu mpaka sita na faini ya shilingi laki 5.

Lakini mchezaji Juma Nyosso  msomaji wa Msumbanews.co.tz  anaweza pia kuhukumiwa kwa kanuni ya 10 inayosema
  • Mchezaji atakayebainika kukutwa na makosa ya utovu wa nidhamu yanayojirudia au mara nyingi (Sugu wa utovu wa nidhamu) atafungiwa kucheza kati ya michezo mitano mpaka kumi na faini isiyopungua milioni 1.
Hizo ndizo kanuni mbili ambazo zinaweza zikatoa Hukumu  kwenye sakata la mchezaji Juma Said Nyosso baada ya kumpiga shabiki anayeaminika kuwa ni wa Simba anayedaiwa alimtolea Lugha za kumuudhi mchezaji Juma Nyosso mara baada ya Mchezo Kuisha.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: