Abiria wanaotumia kivuko eneo la feri wamejikuta wakisota kituoni hapo leo Alhamisi baada ya kivuko kikubwa cha MV Magogoni kupata hitilafu hivyo kubaki vivuko viwili ambavyo vinabeba idadi ndogo ya abiria.
Mwananchi ilifika eneo la kivukoni na kukuta msongamano mkubwa wa abiria wakiwa wanasubiri usafiri huo na wengine wakiamua kuondoka kutokana na kusubiri kwa muda mrefu.
Mmoja wa wasimamizi wa ufundi aliejitambulisha kwa jina moja la Ndunguru amesema tatizo hilo limeanza toka usiku kutokana na MV Magogoni kubeba idadi kubwa ya abiria lazima usumbufu ujitokeze.
“Tatizo limeanza tangu usiku ingawa mimi sio msemaji ila unavyoona mafundi wanaendelea na kazi kuhakikisha tatizo linaisha, kivuko hiki ni kikubwa na kinabeba idadi kubwa ya abiria hivyo kikiaribika lazima usumbufu ujitokeze,” amesema Ndunguru.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: