SeeBait
Majaji nchini Ufaransa wamewalaumu wapiganaji walioongozwa na Rais wa sasa wa Rwanda, Paul Kagame kwa kuilenga na kuiangusha ndege iliyokuwa imembeba Rais wa wakati huo wa Taifa hilo, Juvenal Habyarimana 1994.

Hii ni baada ya upelelezi juu ya suala hilo kukamilika. Upelelezi huo ulikuwa unafanywa na Majaji hao wa Ufaransa juu ya shambulio la kombora lililosababisha kifo cha Rais Habyarimana na baadaye kusabisha kuanza kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda mwaka huo huo.

Hata hivyo Rwanda nayo inawalaumu Ufaransa kwa kushiriki kupanga mauaji ya kimbari. 

Upelelezi huu umesababisha mitafaruku kati ya Rwanda na Ufaransa jambo lililosababisha kuvunja uhusiano wao wa kidiplomasia mwaka 2006.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: