Mshambuliaji Mbaraka Yusuf wa Azam FC atakwenda kupata matibabu nje ya nchi.

Msemaji wa Azam FC, Jaffar Iddi amesema uongozi wa klabu hiyo, baada ya kupata majibu ya vipimo vyake, kesho ataondoka nchini kwenda Afrika Kusini.

“Majibu yanaonyesha ameumia meniscus kama ambavyo nilieleza awali. Hivyo atakwenda Afrika Kusini kesho kwa ajili ya matibabu,” alisema.


Mbaraka aliumia wakati akiitumikia timu ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars wakati akiitumikia katika michuano ya Chalenji.

Awali kulikuwa na taarifa kwamba Azam FC ilimtelekeza, jambo ambalo baadaye lilikanushwa na klabu ya Azam FC kwamba imekuwa ikiendelea kufuatilia hali yake.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: