Wakati Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda akiwakarabisha Kundi la Madaktari Bingwa ambao ni Askari wa Kikosi cha Maji kutoka Jeshi la Jamhuri ya watu wa China nchini Tanzania ambao watakuja Tanzania na Meli kubwa ya Kikosi cha Wanamaji kutoka Jamhuri ya watu wa China wakiwa zaidi ya Wanajeshi na Madaktari *380* ikiwa ni Utekelezaji wa Kauli ya *Balozi wa China* aliemaliza muda wake nchini, ambapo alimhakikishia Mhe Makonda kuleta Timu ya Madaktari Bingwa watakaokuja kumsaidia katika juhudi zake za kutoa Huduma bora za Afya kwa Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wasiokuwa na kipato *KIKUBWA* cha kumudu gharama za matibabu.

Kutokana na Uwepo wa Madaktari Hao, *Mhe Makonda* ametangaza tena Kuanza kwa Zoezi jingine la kutoa Matibabu Bure, pamoja na vipimo *BURE* kwa Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam Kuanzia Tarehe 19 mpaka 25 mwezi huu (19-25/11/2017) matibabu ambayo yatatolewa Ndani ya Meli ya Kichina itakayoweka Nanga katika Bandari ya Dar es Salaam.

Pamoja na kutoa Matibabu Meli hiyo pia itatoa Huduma za  upasuaji mdogo na mkubwa pamoja na kutoa dawa kwa watakaobainika kuitaji dawa, watakuja na baadhi ya vifaa vya kusaidia kutengeneza Mashine zetu za x Ray na vipimo vingine ambazo ni mbovu katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Mhe Makonda amewataka wananchi kujitokeza kwa winging katika kuchangamkia *FURSA* ya Matibabu Bure kutoka China.

Katika hatua za awali za Utoaji wa matibabu Bure baadhi ya Watu wasiokuwa na Nia njema WALIBEZA jitihada za Makonda za Utoaji wa Huduma za Matibabu na upimaji *BURE* , lakini sasa Dunia imetambua na kuamua kumuunga mkono katika Juhudi zake za kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wanapata huduma bora za Afya kwa Gharama nafuu
Share To:

msumbanews

Post A Comment: