DSC_0539

NA CHRISTINA MWAGALA,OFISI YA MEYA WA JIJI
MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita ameondoka Nchini usiku wa kuamkia leo kuelekea Nchini Ujerumani kuhudhuria mkutano wa mameya wote Duniani unaofanyika nchini humo.
Meya Mwita ameondoka Nchini hapa akiwa ameambatana na Mkugenzi wa jiji Spora Liana ,Afisa Mipango miji wa jiji, ambapo watakuwa nchini humo kwa muda wa siku nane na kurejea jijini hapa Novemba 15.
Meya Mwita amehudhuria mkutano huo wenye lengo la kujadili suala la mabadiliko ya tabia ya nchi hususani katika kukabiliana na janga la mafuriko kwenye maeneo ambayo hukumbwa  na changamoto hiyo.
Aidha katika mkutano huo, Meya Mwita atatumia nafasi yake kushawishi Umoja wa Mataifa, Mameya sambamba na Taasisi zinazo husika na mabadiliko ya Tabia ya Nchi kusaidia changamoto za mafuriko ambazo zimekuwa zikilikabili jiji la Dar es Salaam.
Meya Mwita alisema kuwa kupitia mkutano huo, wakazi wa jiji la Dar es Salaam wategemee mabadiliko makubwa katika suala zima la utatuaji wa changamoto ya mafuriko.
Hata hivyo baada ya kumaliza kwa mkutano huo atakunata na kufanya mazungumzo na Meya wa jiji la Hamburg ambapo awali walikuwa na makubaliano ya kuboresha miundombinu ya kuhifadhia takataka katika halmashauri ya Kinondoni (Dampo).
Share To:

msumbanews

Post A Comment: