Mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi Mkoani Mwanza, Peter Saramba na Mpigapicha Michael Jamson wamepata ajali eneo la Kimbu B, Wilaya ya Bariadi wakiwa wanatoka Simiyu kwenye sherehe za maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julias Kambarage Nyerere zilizoambatana na kuzima mwenge.

Akizungumza na gazeti hili muda mfupi baada ya ajali hiyo, Saramba alisema  watu wawili wamefariki papohapo katika ajali hiyo wakati yeye akiwa amelazwa katika hospitali ya Mkula Wilaya ya Busega akipatiwa matibabu kufuatia majeraha aliyoyapata..

“Ajali ilikuwa mbaya sana,ila namshukuru Mungu nipo mzima ingawa nimepata majeraha madogomadogo, lakini tumeletwa hapa Busega katika hospitali ya Kikula kwa ajili ya kupatiwa matibabu, na tayari madaktari wanatuhudumia hapa” alisema Saramba.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: