CHAMA  cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe kimesema kuwa kinaungana na viongozi wengine wa vyama vya habari hapa nchini ili kuishawishi kamati ya bunge kuto upitisha Muswada wa sheria ya huduma za habari ili kuusogeza mbele na kuwapa waandishi wa habari kuujadili kwa kina.

Muswada huo unatarajia kupitishwa na bunge linalotarajiwa kuanza Mwishoni mwa Oktoba ambapo mpaka sasa Baadhi ya waandishi mikoani hawajaupitia na hawajatoa maoni yao.

Akizungumza na waandishi wa habari katibu wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe Khamis Kasapa amesema kuwa muswada huo ukipitishwa unamaslahi kwa waandishi wa habari licha ya baadhi ya vipengele kuwabana waandishi.




Muswada huo wa huduma za habari ukipitishwa umebeba maslahi ya waandishi wa habari, na uhuru wa kupata habari na baada ya kujadiliwa kwa mara ya pili unatarajia kupelekwa mbele ya Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Magufuli kwaajili ya kuupitisha na kuwa sheria.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: