SHIRIKA la kimataifa la British Council limesema vijana wengi nchini Tanzania wanaishi wakiwa na hofu na mashaka kutokana na kutokuwa na uhakika wa kuweza kuzitimiza ndoto zao kunakotokana na ukosefu wa ajira, mitaji na uelewa mdogo wa fursa zinazopatika serikalini.

Akizungumza kwenye kongamano la kupaza sauti lililowakutanisha vijana zaidi ya 150 wa Dodoma mjini katika ukumbi wa Saint Gasper Mkurugenzi wa Mipango na Miradi wa Shirika hilo Nchini Tanzania Nesia Mahenge  alisema changamoto iliyokubwa ni vijana kukosa taarifa ambapo ni asilimia nne tu kati ya 3000 waliohojiwa ambao wana taarifa za fursa zilizopo serikalini

Mkurugenzi huyo alisema shirika hilo liliwahoji jumla ya vijana 3000 katika mkoa 6 ya Dar es laam, Mwanza, Arusha, Mtwara, Zanzibar na Dodoma ambapo hata hivyo wamebaini kwa sasa wengi vijana wameamka na kila mmoja ana wito wa kutaka kusimama na kujisaidia mwenyewe katika kujiletea maendeleo

Mahenge alisema vijana hao wanakwamishwa na ukosefu wa Ajira, Fedha za Mitaji, viwango duni vya elimu na kutokuwa na ujuzi  hali inayowafanya kuishi kwa Hofu, mashaka na wasiwasi wa kutojua ni kwa namna gani watatimiza malengo yao ya kimaendeleo

“vijana hao 3000 waliorodhesha changamoto mbalimbali zinazowakwamisha huku jambo lingine likiwa rushwa ikiwemo ya ngono  

Tatizo lililokubwa ni vijana kutokuwa na taarifa za kutosha kuhusu fursa mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na serikali ikiwemo ruzuku za kuwezesha vijana mfono ukiwa kwa idadi hiyo ya vijana tuliowahoji ni asilimia 4 pekee ndiyo wenye taarifa”, alisema

Aidha aliwataka vijana kupaza sauti ikiwemo kuwa na mijadara na serikali ili hatimaye waweze kusaidiwa

Mgeni Rasmi katika Kongamano hilo alikuwa Mbunge wa Jimbo la Chilonwa lililopo  wilayani chamwino Mkoani humo Joel Mwaka ambaye aliwataka vijana hao kuanzisha au kujiunga katika vikundi vilivyopo ili iwe rahisi kwa serikali kuwaona na katimaye kuweza kuwasaidia kurahisi kuliko kila kijana akawa kivyake ambapo hata hivyo aliwakumbusha wakuu wa wilaya na mkoa kuitekeleza agenda ya kutenga maeneo ya ardhi kwa ajili ya vijana

Share To:

msumbanews

Post A Comment: