Katika kuelekea maazimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere octoba 14 kila mwaka, Umoja wa vijana wa CCM mkoa wa Arusha (UVCCM) umeamua kuienzi kumbukumbu  hiyo kwa kujitolea Damu  itakayosaidia kuokoa maisha ya watu wenye uhitaji wa damu

Akizungumza katika zoezi hilo la uchangiaji damu lilofanyika katika Ukumbi wa Makao makuu ya CCM mkoa wa Arusha Mjumbe wa Baraza kuu la UVCCM Taifa Zeloti Saitoti amesema kuwa wao kama umoja wa vijana wameamau kumuenzi baba wa taifa kwa kuchangia damu japo alituhimiza kupigana vita na maradhi, umaskini pamoja na ujinga



Akizungumza wakati wa utoaji  damu  Afisa maabara kutoka Halmashauri ya wilaya ya Arusha kitengo cha Damu salama Joseph  Mpanda amesema kuwa zoezi hili la umoja wa vijana  UVCCM  kujitolea damu limekuja kwa wakati muafaka kwa maana kwa sasa hapa nchini kuna uhitaji mkubwa sana wa damu


Aidha  kwa upande wake mwenyekiti wa umoja wa wanawake  ya chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha (UWT) Flora Zelote   ambaye alikuwa wa kwanza kuonyesha  uhamishashaji huo wa kujitolea damu amesema kuwa wao kama jumuiya ya wazazi wameelewa umuhimu mkubwa wa kuchangia damu ndio maana wakaamua kujitokeza katika zoezi hilo



Wakati huo katibu mkuu wa shirikisho la  vyuo vikuu mkoa wa Arusha chama cha Mapinduzi  Agness Mchau  amesema kuwa wamekuja kushirikiana na UVCCM  wao kama wanafunzi  na kuwataka vijana wote wa mkoa wa Arusha kujitokeza  kuchangia damu ili kuokoa maisha ya watu wenye uhitaji wa damu
Isert SHIRIKISHO
Share To:

msumbanews

Post A Comment: