Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Leila Muhaji akizungumza na waandishi wa kuhusu wizi huo wa vifaa vya umeme vyenye thamani ya milioni 61 na kukamatwa,Kulia ni Naibu Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya.

 Gari la Tanesco likiwa na shehena ya vifaa vilivyoibwa  Kikuu cha Polisi Dar es Salaam.

 

Tarehe 18-10.2016 saa 10;00 jioni maeneo ya Salasala Mkoa wa Kipolisi Kinondoni Polisi wakishirikiana na Kikosi kazi cha kuzuia uharibifu wa miondo mbinu ya Shirika la umeme Tanzania 

Tanesco lilipata taarifa toka kwa raia mwema kuwa kuna watu wanaohujumu miundo mbinu ya Shirika hilo. 

 Kikosi hicho kilifika eneo hilo katika nyumba ya Willfred Barutti (45) mkazi wa Makumbusho na kufanya upekuzi kwenye nyumba hiyo ambapo walivipata vifaa mbalimbali Line Meterial ambavyo hutumika kwa ajili ya kuunganisha umeme vya Kampuni ya Tanesco.

Polisi waliwenda katika nyumba nyingine mali ya Betrice Emmanuel (42) mkazi wa Salasala Mabanda wakafanya upekuzi na kufanikiwa kukamata vifaa vifuatavyo;

Nyaya aina yka Drums'02,roller ya waya aina ya AICC ya umeme wa 50 mm ambazo hutumiwa na tanesco kituo cha Kilimahewa huko Kawe Wilaya ya Kinondoni

Thamani ya vifaa hivyo vinakadiliwa kuwa Tsh.61,000,000,Watuhumiwa wawili wanashikiliwa kwa mahojiano na Upelelezi utakapokamilika tapelekwa mahakamani kwa hatua za kisheria.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: