UCHUMI WAENDELEA KUIMARIKA NCHINI .
Gavana wa Benki Kuu (BoT), Benno Ndulu amesema hali ya uchumi wa
Taifa ni nzuri na itaendelea kuimarika zaidi mwaka huu na kufikia ukuaji
wa asilimia 7.2.
Ndulu amesema kuna
viashiria vingi vinavyoonyesha kwamba hali ya uchumi ni nzuri. Viashiria
hivyo ni kuingezeka kwa uzalishaji wa umeme, uzalishaji na matumizi ya
cement, kuongezeka kwa uagizaji wa malighafi nje na makusanyo ya kodi.
Anasema miradi mikubwa
ya uwekezaji inayotarajiwa kuanza mwaka huu pia itaongeza kasi ya kukua
kwa uchumi. Miradi hiyo ni ujenzi wa reli ya kati, upanuzi wa bandari
ya Dar, ujenzi wa bomba la mafuta na upanuzi wa viwanja vya ndege.
“Miradi hiyo itatoa
fursa nyingi za ajira, matumizi ya cement yatakuwa makubwa, pia
utaimarisha sekta ya usafirishaji ambayo inakua kwa asilimia 7.9”
amesema Ndulu.
www.msumbanews.bogspot.com
Back To Top
Post A Comment: