PAMOJA na serikari na wadau kufanya juhudi za kuelimisha wafugaji wa wanyama mikoa ya nyanda za juu kusini wafugaji hao wanakosa huduma kutoka kwa wagani ambao wanadaiwa kufanya kazi kwa kusuasua na kuchelewa kutoa huduma wanapo hitajika.

Wafugaji hao wamesema kuwa pamoja na kukosa huduma muhimu za matibabu na ushauri kwa shughuli zao za ufugaji wanaomba serikali kuongeza wagani katika vijiji vyao ili kufuga kwa tija kutokana na elimu wanayoipata kila wakati.


Wafugaji wanaomba serikali kuwasambazia wagani vijijini kwao wakati wakipatiwa elimu ya kuzitambua fursa za kujiongezea kipato yanatolewa na shirika la umoja wa mataifa la biashara UNCTAD,

Wafugaji 40 kutoka mikoa miwili ya Njombe na Mbeya Kwenye halmashauri tano za Rungwe, Wangingombe, Makambako mji, Njombe  mji na halmashauri wilaya, wanatambua fursa za kibiashara zinazotokana na mazingira wanayo ishi.

Serikali nayo inasema kuwa nifaraja kubwa mfugaji wanapo ongezeka kiuchumi.

Mkufunzi kutoka UNCTAD amesema wafugaji hapo awali walikuwa hawana uwezo wa kulitosheleza soko la maziwa ndio maana mafunzo yanatolewa mara kwa mara.


Share To:

msumbanews

Post A Comment: