Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe John Ernest Palingo 

 Meneja maradi wa TACEI Isac Mushi

Diwani kata ya Mlowo Sebastian Kilindu akionyesha chamzo pekee cha maji kilichobakia





 Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe John Ernest Palingo amesimamisha uchimbwaji wa bwawa la samaki na umwagiliaji Kitongoji cha Migombani kijiji cha Mbimba Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe kwa kukiuka taratibu za kisheria.

Palingo ametoa agizo hilo baada ya kupata taarifa kwenye radio na wananchi juu ya uharibifu wa mazingira hivyo  kufanya ziara ya kushitukiza eneo hilo na kuamua kusitisha ili kufanya uchunguzi wa vibali vilivyotolewa na Afisa mazingira Wilaya ya Mbozi Hamisi Nzunda February 18 mwaka huu kufuatia ombi la kikundi cha ufugaji na umwagiliaji cha Isinizya baada ya ombi la February 15 mwaka huu la kuomba uchimbaji wa bwawa.

 Palingo amesema kuwa barua ya Mwenyekiti wa wa kikundi hicho Jackson Mwapua ni batili kwa kuwa haikuwashirikisha wananchi wala mamlaka ya maji, aidha muda wa kuridhia ombi hilo ni dhahiri unatia shaka ndani ya siku mbili kupitisha mradi mkubwa kama huo .

 Kwa upande wake msimamizi wa Mradi huo Julius Mbembela amesema walipata baraka zote kutoka ofisi ya kijiji ingawa hakuweza kuonesha mukhtasari wa kikao hicho cha maridhiano . 

Mwenyekiti wa kitongoji cha Migombani  Monica Ngondya amesema yeye hautambui mradi huo na wananchi wake hawajawahi kushirikishwa chochote.

Naye Diwani wa Kata ya Mlowo Sebastian Kilindu amesema yeye kama msimamizi wa maendeleo wa Kata hajawahi kupata taarifa ya ombi la mradi huo bali alipopata malalamiko ndipo alitembelea eneo hilo na kushuhudia uharibifu wa miti ya asili na vyanzo viwili kati ya vitatu ambavyo vitasababisha kukosekana maji kwenye bwawa la TACRI Mbimba ambalo ndilo husaidia usambazaji wa maji kwa ajili ya matumizi kwa wakazi wa Vwawa na vitongoji vyake. 

Naye Meneja wa TACRI Isaac Mushi amesema bwawa la TACRI limejengwa mwaka 1946 hivyo kuruhusu bwawa hilo kujengwa kungesababisha kituo hicho cha utafiti kufungwa kwa ukosefu wa maji. Baada ya kujiridhisha na ziara hiyo Mkuu wa Wilaya Palingo alitoa agizo la kusimamishwa mradi huo na kumwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi kukaa na mamlaka zote ili kulipatia ufumbuzi mgogoro huo na kwamba hatakuwa tayari kufumbia macho kuona taratibu zikivunjwa na hatasita kumchukulia hatua za nidhamu endapo atabaini ukiukwaji wa sheria.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: